KAWAIDA ATAKA MABADILIKO NDANI YA UVCCM.
Na Mussa Augustine.
MAKAMU Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa Mohamed Kawaida amemuagiza Katibu Mkuu Mpya wa Umoja huo Fakii Lulandala kuhakikisha analete mabadiliko ya kiutendaji ndani ya Taasisi hiyo.
Aidha Mweyekiti huyo Taifa wa UVCCM amesema Kama Mtendaji Mkuu wa UVCCM Taifa anapaswa kuhakikisha anawasimamia Watendaji wengine wote katika ngazi mbalimbali ikiwemo wa mikoa na Wilaya ili kufanya Umoja huo uzidi kuimarika kiutendaji nchi nzima.
Aidha amesema Mabadiliko ndani ya UVCCM hataweza kuyafanikisha pasipo na ushirikiano na watendaji wengine, hivyo ametakiwa kushirikiana nao bega kwa bega.
Kawaida amemwagiza pia kuhakikisha Idara ya Chipukizi inakuwa imara kwa kuhakikisha anakuja na mpango wa Wiki ya Chipukizi ambayo Chipukizi wataitumia kuwasilisha changamoto zao na maoni yao kwa maendeleo ya chama.
Kadhalika Kawaida amemtaka Katibu Mkuu huyo kuandaa mpango wa kushugulikia Kero za vijana ambao ni Wakulima, wanafunzi, wajasiriamali, wavuvi, wachimbaji wadogo wadogo na kadhalika ili kupigania maslahi yao na kuwainua kiuchumi.
"Hivyo tushughulike na makundi haya na kushughulikia changamoto zao," ameeleza Kawaida.
Vile vile Kwaida amemuelekeza Katibu Mkuu
kuandaa mpango kazi wa kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi juu ya
vijana.
Nae Makamu Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Rehema Sombi amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mengi na makubwa ikiwemo kuwawezesha vijana kwa kiasi kikubwa kwani amewatoa mtaani na kuwapeleka saiti kwenye kilimo, ajira, mikopo kutoka mfuko wa uwezeshaji na kadhalika.
Aidha ameeleza kuwa baada ya miezi minne kupita bila safu ya uongozi wa UVCCM Taifa kukamilika, sasa imekamilika baada ya uteuzi wa Katibu Mkuu huyo Lulanda
Hakuna maoni
Chapisha Maoni