GALCO INSURANCE KUTOA HUDUMA YA BIMA YA “TAKAFUL”
Na Mussa
Augustine.
Naibu
Kamishina wa Mamlaka ya Bima nchini (TIRA) Bi.Khadija Said amezitaka
wakala zinazotoa huduma za bima kutoa huduma hiyo kwa kuzingatia sheria na
kanuni zilizotolewa na mamlaka hiyo..
Kauli hiyo ameitoa
Oktoba 5,2023 jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Bima ya TAKAFUL
inayotolewa kupitia kampuni ya uwakala ya GALCO Insurance kwa kushirikiana na
kampuni mama ya ZIC TAKAFUL LTD ambayo ni huduma ya bima yenye misingi na
Sheria za kiislam .
Bi . Khadija
amesema kuwa kampuni zote za uwakala wa bima zinapaswa kuzingatia kanunu na
sheria zilizowekwa na TIRA iliwaweze kitoa huduma kwa wateja wao kwa
kiwango na ubora unaotakiwa kwa mujibu wa sheria.
Aidha
ameendelea kufafanua kuwa kwa mujibu wa mpango wa kuendeleza sekta ya fedha
hadi kufikia mwaka 2030 matumizi ya bima yamelengwa kufikia asilimia 50 lakini
mpaka sasa matumizi hayo ni asilimia kumi na tano pekee nakwamba uelewa wa
matumizi ya bima umelengwa kufikia asilimia 80 mwaka 2030 ambapo kwa sasa .
Hata hivyo Bi. Khadija amezisisitiza kampuni na wakala za bima kuendelea kutoa elimu kwa watanzania waweze kuchangamkia kujiunga na huduma za bima kwani zinasaidia kutatua changamoto wanazoweza kukumbana nazo wakati wanapokubwa na majanga ya aina mbali mb
"Huduma
hii ya Bima ya Takaful mchakato wake umeanza rasmi mwaka 2008
kupitia kampuni ya ZIC Insuarance na imezinduliwa rasmi miezi
mitatu iliyopita na Rais wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt
Hussein Mwinyi,hatua hii ni kutokana na kuwepo kwa mahitaji makubwa ya
Bima ya Misingi ya hesheria ya kislam"TAKIFUL ) lakini huduma hii
inatolewa kwa waislam na wakristo kwa ujumla"amesema
Takaful
ambayo inasimama kama nguzo katika jamii na inasimama katika misingi ya
kushirikiana pale ambapo kutakuwa na majanga au faida.
Kwa upande
wake Mkurugenzi wa makampuni ya GSM Group yanayomiliki kampuni ya
Galco Insuarance Ltd ,Benson Mahenya amesema huduma zao za bima ya Takaful sio
sera ila ni ahadi ya kuwa wapo karibu na watu katika kutatua changamoto za
kibiashara na kimaisha kiujumla .
"Tunafanya
kazi katika misingi ya kweli na uwazi na kuhakikisha usawa katika utoaji wa
huduma,tuna uzoefu wa miaka mitano sokoni na katika kipindi hiki tumeweza kutoa
huduma kwa watu binafsi zaidi ya mia tano na makampuni zaidi ya kumi
,"amesema Mahenya .
Naye meneja
Biashara Emmanuel Bugabu amesema kuwa Galco Insurance Brokers
inashirikiana na makampuni mbali mbali ya kiwemo MAYZUH COMPAZNY LIMITED
ilikutoa mafunzo kwa wafanyakazi na kuhakikisha wana uelewa na huduma ya
Takaful na wanashirikiana na pia na ZIC TAKAFUL LTD katika utoaji huduma hiyo
ya bima ya misingi ya kiislam TAKAFUL.
"Nia yetu ni kukuza mwamvuli wetu wa huduma za bima kwa watu wote wakiwemo mtu mmoja mmoja , wanafamilia,wafanyabiashara na makampuni au taasisi mbali mbali,nakusisitiza kuwa wafanyakazi wa Galco Insuarance wamepata elimu ya kutosha kutoa huduma kwa wateja" amesema Bugabu.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni