CODECO KWA KUSHIRIKIANA NA TFS WAANDAA MATEMBEZI HIFADHI YA KAZIMZUMBWI, KUYATUMIA KUADHIMISHA MIAKA 24 KIFO CHA NYERERE
NA MWANDISHI WETU
TAASISI ya Uhifadhi wa Mazingira (CODECO) kwa kushirikiana na Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) wameandaa Matembezi katika Hifadhi ya Kazimzumbwi wilayani Kisarawe ikiwa ni sehemu ya kumbukizi ya miaka 24 tangu kifo cha baba wa Taifa Hayati Julius Nyerere.
Akizungumza na waandishi wa habari Oktoba 4, 2023 jijini Dar es Salaam Afisa wa TFS Catherine Melchiory amesema kwa kila mshiriki wa Matembezi hayo atapaswa kulipa gharama ya shilingi 35,000.
“Gharama ni 35,00 ikijumuisha chakula, usafiri, Burudani yani Live Band, ngoma za asili na Ma Dj wa Burudani,” amesema Catherine
Aidha amebainisha kwamba mgeni Rasmi wa Matembezi hayo anatarajiwa kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Angella Kairuki.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni