Zinazobamba

Dkt Khalid: Daktari wa Mufti wa Tanzania aliyebobea kwenye tiba lishe



 

Mwandishi wetu, Dodoma

Matatizo ya afya ya akili ni moja ya changamoto kubwa katika jamii tunayoishi, inaelezwa kuwa ndani ya mwezi mmoja si ajabu kusikia mtu ameondoa uhai wake au ameondolewa uhai wake kutokana na matatizo ya akili

Utafiti ambao sio rasmi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa kuna kuongezeka kwa matukio yanayotokana na afya ya akili, kumekuwa na matukio ya kusikitisha yanayohusisha afya ya akili.


Kule Jijini Mwanza, dada mmoja anayekadiliwa kuwa na miaka 24, Bi Asteria Wilberd maarufu Mgole akiwa na mtoto wake wa miezi 4 alidaiwa kupotea, chanzo kikitajwa kuwa ni matatizo ya afya ya akili yaliyo muanza takribani miezi minne iliyopita

Pia mitaani takwimu ambazo sio rasmi zinaonyesha kumekuwa na ongezeko la watu wenye changamoto ya afya ya akili, hususani vijana ambao wamejikita katika michezo ya Kamari na uraibu

Si ajabu siku hizi kumkuta kijana akizungumza peke yake njia nzima, ukibahatika kumuhoji utagundua kuwa changamoto kubwa inayomsumbua ni akili yake kuingiliwa na mambo mengine.

Hakika hakuna jambo baya kama kuharibu akili, utakubaliana na mimi kuwa akili ni kitu chenye thamani kubwa, ukiondoa thamani ya nafsi kitu ambacho kinafuata ni akili.

Licha ya umuhimu huo bado kumekuwa watu wanaharibu thamani hiyo kwa nguvu zote.

Mmoja wa wataalam wa tiba lishe na daktari wa Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir, Dkt Khalid Hussein amekili kuwa tatizo la afya ya akili limezidi kuwa kubwa na kwamba kama hatua stahiki hazitachukuliwa basi kuna hatari kubwa.

Dkt Khalid ambaye anauzoefu wa tiba lishe kwa Zaidi ya miaka 22 mpaka sasa, amesema maatatizo makubwa ya watu hadi kufikia kuharibu akili zao ni kuacha kufuata maamlisho ya Mwenyezi Mungu na kuamua kuishi kwa uhuru wanaoutaka, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limeleta hatari na kuharibu akili.

Dkt Khalid ambaye hakusita kueleza ndoto yake ya kutibu wagonjwa wa uraibu kwa mwezi mmoja kupitia tiba lishe, amesema anajisikia vibaya kuona watu wanaendelea kuharibu akili ambayo Mwenyezi Mungu amewazawadia. Fuata kiungo hiki kwa faida zaidi kuhusu Dkt huyu

Daktari wa Mufti wa Tanzania aliyebobea kwenye tiba lishe

“Mimi ni Daktari wa tiba lishe, ninafanya tafiti lakini pia ninatatibu magonjwa ambayo tayari nimeyafanyia utafiti, nashukuru Mufti ameona kazi inayofanyika na ameamua kuniteua kuwa daktari wake,” alisema

Pia, Dkt Khalid ambaye ni msomi wa dini kwa ngazi ya thanawi aliyeipata huko Doha/Qatar amewaomba watanzania kuacha tabia ya kubeza tiba mbadala akisisitiza kuwa kwa miaka ambayo amefanya kazi ameweza kusaidia watu wengi na kupona.

“Wapo watu wachache ambao wanabeza tiba asili, lakini nataka niseme wazi kuwa watu hao elimu bado haijawafikia, hapa nchini kunahatua zimepigwa ikiwamo baadhi ya hosptali za serikali kuanza kutumia dawa hizi ikiwamo Hospitali ya Benjamini Mkapa ya Jijini Dodoma,” alisema

Akieleza historia yake katika kazi ya utabibu na utafiti wa dawa lishe, Dkt Khalid amesema ameanza kazi toka mwaka 2001 akiwa nchini Afrika Kusini katika mji wa Cape town, kitongoji cha Kairisha.

Kisha, alipata fursa ya kuzunguka nchi mbalimbali kufanya tafiti zake ikiwamo Botswana katika mji wa Gaborone, Malawi katika mji wa Lilongwe na Congo katika Mji wa Lubumbashi


Nchi zingine ambazo amefanikiwa kwenda ni pamoja na Visiwa vya Comoro katika mji wa Moroni, Pemba na Msumbiji katika mji wa Maputo.

“Upande wa elimu sijasoma sana elimu ya sekula zaidi nimejikita katika masomo ya kiimani, nimesoma sana quran hadi ngazi ya chuo Kikuu, nimesoma nchini Qatar, Doha huko Falme za Kiarabu,” alisema

Aidha akieleza ilikuaje mpaka akajiunga na fani hiyo, Dkt Khalid alisema wazo la kutoa huduma hiyo lilikuja baada ya kugundua kuwa kuna wagonjwa wengi wanateseka kupata tiba ya uhakika kwa baadhi ya maradhi, kwani hospitali hazina uwezo wa kutibu baadhi ya magonjwa bali wanapunguza makali yake tu.

Ametaja mfano wa maradhi ambayo yanasumbua watu sana lakini hayana tiba ya uhakika katika hospitali za kawaida ni pamoja na maradhi ya vidonda vya tumbo na Asma (Pumu).

Pia, Dkt Khalidi ameeleza kufurahishwa kwake kwa kupatiwa nafasi na Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania ya kuwa Daktari wake kwani nafasi hiyo ni nyeti na ameahidi kuisemea tasnia ili wachache ambao bado hawajapata faida ya kujua thamani ya tiba lishe wapate kuelimika.

“Badhi ya mambo ambayo yamenifurahisha katika kazi yangu ni kuaminiwa na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir, kwa kweli sio jambo dogo, ameniheshmisha katika jamii lakini pia amejibu kwa vitendo kuwa anathamini kazi zinazofanywa na wasomi wa tiba lishe,” Alisema

 

Hakuna maoni