Zinazobamba

TANESCO IMEANZA KUTEKELEZA MIRADI MBALIMBALI YA UZALISHAJI WA UMEME JADIDIFU


                           Waziri Mkuu Kassim Majaliwa 
Na Mussa Augustine

Shirika la Ugavi wa Umeme Nchini(TANESCO) limeanza utekelezaji wa Miradi Mbalimbali ya Uzalishaji wa umeme jadidifu ili kuongeza mchango wake katika gridi ya Taifa na kuweza kuondokana na changamoto za Nishati hiyo.

Akizungumza na Waandishi wa habari katika Kongamano la tano la kimataifa la maonyesho ya Nishati Naibu Mkurugenzi wa Uwezeshaji wa shirika hilo Declan Mhaike amebainisha kuwa miradi saba ya umeme jua   na Upepo ya Megawati 170 hadi 100.

Amesema miradi hiyo itaongeza mchango wake katika gridi ya Taifa kutoka asilimia 0.5 ya sasa hadi asilimia 20 ifikapo mwaka 2025 nakuwezesha kuwa na umeme wa kutosha.

Aidha Mhaike ameendelea kusema kuwa miradi inayoendelea kutekelezwa ni pamoja na wa megawati 100 wa upepo iliyopo Makambako Mkoani Njombe, Mradi wa megawati 100 wa Upepo uliyopo Ismani Mkoani Iringa,pia Megawati 60 za Umeme jua uliyopo Dodoma,na Megawati 100 za umeme jua uliyopo Manyoni Mkoani Singida.

Mhaike ameendelea kufafanua kuwa Mradi mwingine unaotarajiwa kutekelezwa ni ule wa Kituo Cha Kishapu Mkoani Shinyanga ambao utazalisha megawati 50 hadi 150 ,huku kuna mradi mwingine utakaotekelezwa Wilayani Same Mkoani Kilimanjaro.

Awali katika kongamano hilo lililofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa Mwalimu Julius  Nyerere(JNICC) jijini Dar es salaam Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alisema kwamba Serikali imejidhatiti kutekeleza vyanzo vingine vya umeme na sio kutegemea umeme wa Maji pekee na kwamba Tanzania ina mpango wa kua mzalishaji Mkubwa wa Nishati ya Umeme Duniani.

"Lengo letu tunataka tuwe wazalishaji wakubwa wa umeme kupitia rasilimali tulizonazo tuweze kua na umeme wa kutosha ,rahisi lakini pia unapatikana wakati wote,na ikiwezekana tuuze nje ya nchi ,hayo yote yatafikiwa kupitia mjadala huu wa mwelekeo wa namna tunavyoweza kuzalisha" amesema Waziri Mkuu Kassim Majaliwa

Kwa upande wake Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt Dotto Biteko amesema kwamba Uchumi wa Tanzania unazidi kukua hivyo Nishati ya Umeme inahitajika kwa kiasi kikubwa hivyo vyanzo vya umeme vinatakiwa kuongezwa ili kuwa na umeme wa uhakika.

" Tunafahamu kua Uchumi ni Mkubwa kwa Watu wetu lakini vyanzo vya umeme bado ni vilevile lazima tuongeze vyanzo vingine ili kua na umeme wa uhakika kwa ajili ya shughuli zetu za Uchumi" amesema Dkt Biteko.

Kwa Mujibu wa Wizara ya Nishati  fursa ya uwekezaji kwa  Makampuni binafsi inakadiriwa kuwa asilimia 78 kwa ushiriki wake,kuwekeza katika miradi ya Nishati Jadidifu yenye thamani ya shilingi trilioni 89  katika fursa za uwekezaji wa jumla ya Megawati 490 ambazo ni Upepo Megawati 150,umeme jua megawati 205 na joto ardhi megawati 135 hali hiyo itasaidia kua na umeme wa uhakika.

Hakuna maoni