Zinazobamba

JUKATA LIMEIOMBA SERIKALI KUACHANA NA MPANGO WA KUTOA ELIMU YA KATIBA MPYA KWA MIAKA MITATU.


                Mkurugenzi Mkuu wa (JUKATA) Bob Chacha Wangwe

Na Mussa Augustine.

Jukwaa la Katiba Tanzania JUKATA limeiomba Serikali kuanchana na Mpango wa kutoa Elimu ya Katiba ya mwaka 1977 kwa miaka mitatu kama ilivyotoa msimamo huo kupitia aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Dkt Damasi Ndumbalo badala yake ipeleke miswada ya Sheria za michakato wa katiba Bungeni kwa ajili ya marekebisho.

Akitoa taarifa kwa  Waandishi wa habari leo Agost 31,2023  Jijini Dar es salaam Mkurugenzi Mkuu wa (JUKATA) Bob Chacha Wangwe amesema ni vyema serikali kuona umuhimu wa kutumia nyaraka muhimu za mchakato wa katiba Mpya katika kutunga au kurekebisha Sheria za mchakato wa katiba kwakuwa zimezingatia mahitaji ya sasa ya nchi pamoja uzoefu wa mchakato uliokwama mwaka 2014.

"Tunatoa wito kwa Waziri wa katiba na Sheria Balozi Pindi Chana kutoa mapema ratiba za hatua za mchakato wa katiba mpya ili kuondoa sintofahamu ambayo imetawala miongoni mwa Watanzania kwa ujumla " amesema Wangwe

Ameendelea kufafanua  kuwa  JUKATA  bado inaamini hatua iliyotangazwa na wizara ya Katiba na Sheria hivi karibuni ya kutoa Elimu ya katiba kwa miaka mitatu ni hatua ambayo inatakiwa kuangaliwa upya kwani ni ucheleweshwaji wa kuanzisha mchakato wa katiba mpya na kutumia vibaya fedha za watanzania kwani hatua hiyo ilishafanyaika na iliyokuwa tume ya marekebisho ya katiba.

" Ujio wa Balozi Dkt  Pindi Chana katika Wizara ya Katiba na Sheria tunaamini utaleta nuru ya upatikanaji wa katiba na kuondoa vikwazo ambavyo kwa namna Moja ama nyingine vitaweza kutukwamisha kama hilo la kutoa elimu ya Katiba ya mwaka 1977 kwa miaka mitatu " amesema 

 Nakuongeza kuwa" JUKATA tunampongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassani kumuondoa Dkt Damasi Ndumbaro kwenye Wizara ya Katiba na Sheria kwani tunaamini aliona haja ya kutafuta mtu mwingine kwa ajili ya kumsaidia kumsaidia Wizara hivyo tunaahidi kumpa Ushirikiano lakini pia kumtakia kila heri katika majukumu yake mapya .


                  Mwenyekiti wa Jukata Dkt  Ananillea Nkya

Awali akizungumza Mwenyekiti wa JUKATA Dkt  Ananillea Nkya amesema Mchakato wa upatikanaji katiba mpya kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kutengeneza Sheria  mfano  ambayo itawafanya watanzania wote wajue namna ya kupata katiba mpya .

Dkt Nkya amewasihi  watanzania wote kuwa kitu kimoja katika kupata  katiba mpya kwakuwa jambo hilo halihitaji kuwa na utashi wa kisiasa hivyo linahitaji Uzalendo wa maslahi mapana ya kitaifa.

                    Mjumbe wa bodi ya Jukata Deus Kibamba 

Naye Mjumbe wa bodi ya Jukata Deus Kibamba  amesema Mchakato huo utaendelea  pale ulipoishia   kwa kufuata rasimu ya katiba ya Jaji Warioba kwa kuipeleka kwa wananchi waendelee kutoa maoni yao yatakayofanikisha kupatikana kwa katiba mpya itakayoleta Maendeleo katika Taifa.

Hakuna maoni