Zinazobamba

Mwalongo awaasa watanzania kutunza mazingira, awakaribisha mnazi mmoja, ni katika wiki ya tiba asili ya Mwafrika

 




Katibu wa shirika la dawa asili na utunzaji wa mazingira Boniventure Mwalongo amewataka watanzania kutunza mazingira na kuacha tabia ya kukata miti hovyo kwani miti ya asili ina faida nyingi kwa matumizi ya binadamu.

 

Akizungumza na wanahabari bwana Boniventure Mwalongo amebainisha kuwa kupitia miti ya asili watanzania tumepata faida nyingi ikiwepo kipindi cha covid 19 watu walitibiwa kupitia miti na mimea ya asili kwani miti mingi hapa nchini inatumika kama tiba .

 

Bwana Mwalongo ametoa wito kwa wadau wa mazingira na tiba asili kujitokeza kwa wingi katika kongamano la wadau wa mazingira na tiba asili kujitokeza kwa wingi katika viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 27 mpaka 31 ambapo elimu mbalimbali za tiba za kisuna na tiba asili na mazingira watanufaika.

 

Aidha katibu huyo amefafanua kuwa kupitia mimea na miti ya asili watoa huduma watapata elimu kwani mpaka sasa wamekuwa wakitoa huduma ya kutengeneza dawa kupitia miti ya asili kwa wagonjwa  waliopo katika hospitali za serikali magonjwa kama kansa,covid 19,kisukari,afya ya akili wamepata nafuu kupitia dawa hizo.

 

Kongamano hilo la wiki ya maadhimisho hayo linatarajiwa kuwa na waratibu wa tiba hizo kutoka halmashauri 184 za nchi ya Tanzania,mikoa 26 ya Tanzania bara,vyuo kama Nelsoni Mandela,chuo kikuu cha Dar es salaam,Sokoine,ITN,Nimri na vyuo vingine ambapo pia kutakuwa na mijadalq ya kisayansi inayohusu mchango wa miti ya asili na ufanisi wake na namna ya kwenda kwenye majaribio ya kisayansi.

 

Aidha maadhimisho hayo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa katibu mkuu wizara ya afya ambapo wizara wa afya ndio wasimamizi wakuu wa maadhimisho hayo.

 

Hakuna maoni