Zinazobamba

DIWANI LYOTO AOMBA USHIRIKIANO KWA WANANCHI MZIMUNI KULETA MAENDELEO.

                    Diwani wa Kata ya Mzimuni  Manfred Lyoto

Na Mussa Augustine.

Diwani wa Kata ya Mzimuni Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es salaam Manfred Lyoto amewaomba Wananchi wa Kata hiyo kuendelea kushirikiana katika kupambana na Maadui watatu ambao ni Umasikini,Malazi na Ujinga.

Diwani Lyoto ametoa wito huo Agost 31,2023 wakati akizungumza na Mwandishi wa habari hizi ambapo amesema kwamba lengo kuu la uongozi wake ni kuhakikisha kata ya Mzimuni imepiga hatua kubwa katika shughuli za maendeleo.

“Tumeanzisha taasisi ya kutoa mikopo isiyo na riba ili Wananchi wajikwamue kiuchumi kwa kupata mikopo na kuanzisha biashara lakini tumebadilisha utaratibu umekua Selective kwasababu wengi wao tumegundua wanataka kuchukua mikopo lakini hawapo tayari kurejesha mikopo hiyo” amesema Diwani Lyoto.

Nakuongeza “tumejifunza kupitia mikopo ya asilimia kumi iliyokua ikitolewa na Halmashauri ambapo mpaka sasa ni takribani Bilioni nne au tano hazijarejeshwa jambo ambalo Wananchi wanaikatisha tamaa serikali ambayo ilikua na nia njema ya kuwasaidia Wananchi Kiuchumi.

Aidha amesema kuwa Mikopo hiyo ililenga kuondoa Umasikini na kuwafanya wananchi kupata maendeleo yenye uhakika wa kupata huduma bora za kimaisha  kama vile Chakula na Malazi ,lakini wananchi wengi wanaokopa hawarudishi mikopo hiyo kwa wakati.

 Amesema kua Kata ya Mzimuni ina mpango wa kuanzisha Miradi ya kutengeneza fedha ili kusaidia kuwepo na fedha zitakazotumika kutoa huduma kwa wanachi wa kata hiyo ikiwemo mikopo kwa wale ambao watakua na sifa ya kupata mikopo hiyo.

Akizungumzia kuhusu Mmomonyoko wa maadili kwa Vijana amesema kuwa wanajifunza tabia mbaya kama vile Usagaji  kutokana na Umasikini kwani  wazazi wengi wanaishi chumba kumoja na watoto wao na inapotokea wazazi hao wanafanaya tendo la ndoa unakuta watoto wanangalia hivyo nao wanaenda kufanya majaribio kwa vitendo.

“Kama Wazazi tunapaswa kuja na jibu maalumu la kutatua nchangamoto ya tatizo la umasikini ili wazazi wawe na uwezo wa kuisha kwenye nyumba inayojitoshereza kulingana na ukubwa wa familia”amesema

Diwani Lyoto amesema Chanzo kingine na stori za mtaani ambazo zinazungumzwa na Watu wakiwa vijiweni hivyo watoto wanajifunza na wao wanakumbwa katika kadhia hiyo.

“Zamani Mtu akiwa na umri mkubwa ni ishara yakua na busara kwenye jamii lakini sasahivi hakuna busara,unakuta jitu zima tena lizee kabisa halijiheshimu na badala yake linazungumza manene machafu” amesema.

Akizungumzia masuala mengine ya maendeleo katika kata ya Mzimuni Diwani huyo amesema kuwa wanatarajia kufanya mkutano wa hadhara hivi karibu kwa ajili ya kuwaelezea wananchi pamoja na kukabidhi Vifaa vya michezo kwa timu kumi kwa ajili ya kuendeleza soka katani humo nakuinua vipaji vya vijana.

“Nimeshafanaya mazungumzo China ili kupeleka vijana kwa ajili ya majaribio ya kucheza soka la kulipwa ,tatizo vijana wengi ni wavivu na hili ni janga la Taifa lazima tushirikiane vijana waache uvivu”amesema

Pia ameongeza kuwa “natarajia kutoa bima za afya kwa wazee wapatao mia moja ili kuwawezesha kupata huduma za matibabu bure ,hivyo tuna mambo mengi yakufanya yakimaendeleo naomba wananchi tushirikiane kwa pamoja.


Hakuna maoni