Tamko la TEC kuhusu uwekezaji katika bandari ya Dsm lakosolewa kila kona
Na Mwandishi wetu,
Fullhabariblog
Siku chache
baada ya Baraza Kuu la Maaskofu wa Kikatoriki (TEC) kutoa Tamko lao kuhusu
suala la bandari, watu wengi wamekosoa tamko hilo wakisema limejaa udini na
wengine wakienda mbali kabisa wakisema aliyewasilisha ameongeza maneno yake.
Mbali
na kuongeza maneno katika waraka, pia wadau wanasema Kitima hakuwa uhalali wa
kuwasilisha tamko zito kama hilo kwani tayari alishaonyesha kuchagua upande.
Mmoja wa wadau waliokosoa tamko hilo ni Shemasi George Rugambwa
kutoka Seminari ya Ntungamo, Bukoba, ambaye ametoa waraka maalum wenye maswali
sita akihoji uharaka wa TEC kuleta andiko ambalo lina mapungufu mengi
Shemasi Rugambwa
anasema anaamini ufafanuzi wa Padri Kitima kuhusu tamko la TEC unaweza kuwa na
maneno yake binafsi ya ziada kwani alijipambanua awali kuwa na maslahi na jambo
lenyewe.
Maswali sita anayohoji Shemasi Rugambwa…
Katika andiko lake,
Shemasi huyo kutoka Bukoba, amehoji mambo sita ya msingi, ambayo mpaka sasa
walengwa wameshindwa kujibu hoja na kubaki kulalamika kuwa aliyetoa andiko siyo
Shemasi. Maswali yenyewe haya hapa
1. TEC inafahamu kwamba
mwaka 1992 wakati Serikali inapitisha mfumo wa vyama vingi ulikuwa umekataliwa
na asilimia 77 ya Watanzania? Hata hivyo serikali ikaamua uruhusiwe. Hakuna
kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti ya
Mungu.
2. TEC inafahamu kwamba
mwaka 2001 baada ya matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar na mauaji ya wafuasi wa CUF
mwezi Januari, asilimia kubwa ya Wazanzibari na Watanzania kwa ujumla walitaka
kuwepo na mfumo wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar na SMZ na SMT chini ya
Mkapa haikutaka? Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya
Wengi ni Sauti ya Mungu.
3. TEC inafahamu kwamba
mwaka 2014 maaskofu wote Katoliki Tanzania akiwemo Kardinali Pengo na wasaidizi
wake walipokea mamilioni ya shilingi pesa taslimu na nyingine kwenye akaunti
zao kama Askofu Nzigilwa (milioni 80 benki) na Kilaini (milioni 40 benki).
Inajua fedha hizo zilitoka katika kampuni yenye makando kando ya rushwa ya
kihistoria Tanzania. Wananchi wengi walipiga kelele lakini fedha hizo
hazikurudi wala hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya
Wengi ni Sauti ya Mungu.
4. Padri Kitima anasema
kwa zaidi ya miaka 60 ama toka tupate uhuru bandari yetu haijawahi kuendeshwa
na wageni. Hii ni kauli yake au ya maaskofu wa TEC? Ni kweli TEC haifahamu
kwamba kwa zaidi ya miaka 22 Bandari yetu ya Dar imekuwa chini ya kampuni ya
TICTS ikiendeshwa kwa ubia na kampuni toka Hong Kong (Hutchsons?). Kama
wanafahamu, wanakumbuka wabia wazawa wa kampuni hiyo wanahusika kwenye kuwapa
hela maaskofu kama Rugemalira na IPTL yake walivyofanya? Hili wamewahi
kuwaambia waumini wao katika mimbari za ibada?
5. TEC wanafahamu
kwamba mwaka 1998 kwenye mauaji pale Mwembechai walikufa wasio na hatia na
ilikuwa rai ya mamilioni ya Watanzania kutaka kuwepo na suluhu ya kisiasa?
Hakuna kumbukumbu za kanisa katoliki kupinga na kusema Sauti ya Wengi ni Sauti
ya Mungu.
6. Padri Kitima anasema
wananchi wamelikataa Bunge? Ametumia kipimo gani cha Kikatiba? Maana wananchi
wanalikataa Bunge kwa kutowachagua Wabunge kwenye Uchaguzi. Hii “Vox Populi Vox
Dei” ya TEC imetumia kigezo gani? Wananchi wakikataa Bunge pia si wameikataa
Serikali? TEC inaomba vipi busara ya Mheshimiwa Rais ambaye wakati huo huo
inasema serikali yake imekataliwa? Kuna kuchanganyikiwa na haraka kubwa kwenye
tamko la TEC hata namna lilivyochapwa na kupangiliwa. Inanipa mashaka kwamba
chombo hiki muhimu cha Kanisa kimekubali kutumika kwa maslahi binafsi bila
tafakari ya kutosha.
Je hii “Sauti ya Wengi
ni Sauti ya Mungu” ni wengi wapi hasa? Na mungu anayetajwa hapa ni nani?
Usikute mungu anayetajwa na kusemwa asikilizwe ni mungu au miungu watu
waliokuwa wanaingiza miamala kwenye akaunti za baadhi ya maaskofu wetu na
viongozi wengine wa dini miaka nenda rudi. Tujihadhari. Tusiigawa nchi kupitia
madhabahu,” Alimaliza
Hakuna maoni
Chapisha Maoni