Sakata la uwekezaji wa bandari Dsm… Waislam wamechagua kukaa kimya
Na Mwandishi wetu, Fullhabari Blog
Waislam
wameuchukua waraka wa TEC wenye kurasa 8, wakautaza, wakausoma, wakauchambua
kisha wakabaini kuwa huo ni mtego, wakachagua kukaa kimya. Hivi ndivyo
unavyoweza kusema
Wanafahamu
fika kuwa unapoanza kuandika tamko, inaonekana wazi kuwa unajibu hoja zilizowasilishwa
na TEC, na mantiki hiyo TEC itakuwa imeshinda vita kirahisi sana, watatumia
lugha tamu kuwa suala hili sasa limechukua sura ya kidini kwa hiyo ni vizuri
zoezi la uwekezaji ukasitishwa kwa maslahi ya taifa.
Si
wote wanaoweza kung’amua mtego huo, inahitaji akili kubwa, kwa mamntiki hiyo
nawaona waislam hawatajisumbua kutoa matamko juu ya sakata hili la bandari
wakiamini wazi kuwa serikali makini chini ya mama Samia Suluhu Hassan haiwezi
kuwauza raia wake kama wapotoshaji wachache wanavyotangaza.
Hayo
ni maneno ya mmoja wa wachambuzi wa masuala ya kisiasa ambaye anachipukia kwa
kasi sana Bw. Junaid Haithum wakati akipiga stori na Fullhabari Blog juu ya
Tamko la TEC.
Haithum
ameieleza Fullhabari Blog kuwa kwa vyovyote itakavyo anaona wazi kuwa waislam
hawatakuja na tamko kuhusu bandari.
Haithum
ambaye amekuwa mstari wa mbele kwenye kuyatazama mambo kwa mawanda mapana,
amesema mtego ambao umetegwa na TEC ni kuwataka waislam kujibu andiko hilo na
baadaye ionekane jambo hilo limeingia udini na hivyo kuhalalisha kusitishwa kwa
uwekezaji katika bandari
“Ukiniuliza
kama waislam wanahaja ya kuja na tamko nitakwambia hapa, ni bora wakae kimya
kwa sababu hesabu za TEC ni kuwachokoza waislam ili wajibu hoja na hapo ndipo
watakuja na hoja kuwa zoezi la uwekezaji katika bandari inapaswa kuachwa.
Hivi
karibuni TEC ilikuja na tamko la kutokuunga mkono uwekezaji wa bandari, hata
hivyo wengi wamekosoa andiko hilo wakisema limekuwa general, badara ya kushauri
nini kifanyike katika vifungu lakini wao wameukataa uwekezaji wote. Haikufahamika
mara moja kama chanzo cha kukataa uwekezaji huo ni kwa sababu muwekezaji
anatoka taifa la waraabu au kitu gani.
Ends,
Hakuna maoni
Chapisha Maoni