Zinazobamba

TABIBU MADUHU AIHIMIZA JAMII KUTUMIA VYAKULA VYA ASILI KWA AJILI YA KUEPUKANA NA CHANGAMOTO ZA KIAFYA


Na Mussa Augustine

Jamii imeendelea kukumbushwa kutumia vyakula vya asili Ili kuweza kuepukana na changamoto mbalimbali za kiafya ikiwe afya ya uzazi.

Rai hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa kituo Cha Utafiti na tiba asilia cha NYASOSI tabibu Emmanuel Maduhu wakati akizungumza na Vyombo vya habari ofisini kwake Magomeni jijini humo.

Tabibu Maduhu  amesema kuwa tatizo la uzazi kwa wanandoa wengi limekua kubwa hali ambayo imekua ikisababisha familia na ndoa nyingi kuvunjika kutokana na wanandoa hao kukosa watoto ,hivyo sababu hiyo imekuwa ikichangiwa na mambo mbalimbali ikiwemo mfumo mbaya wa ulaji wa vyakula vya viwandani.

" Matatizo ya Uzazi ni changamoto kubwa kwa kizazi Cha Sasa,ndoa na familia hazina amani kwasababu ya kukosa watoto ndani ya familia,na hili tatizo linapotokea mwanamke ndio anaelaumiwa huku Kumbe ni tatizo la wanandoa wote ,ambapo wanatakiwa kuwaona wataalamu wa afya ili waweze kupatiwa matibabu " amesema tabibu Maduhu.

Nakuongeza kuwa mwanaume anaweza kua anashiriki vizuri tendo la ndoa lakini kumbe mbegu zake za kiume hazina uwezo wa kutungisha mimba ,hivyo wanatakiwa waendesha wakapate vipimo Ili kujua tatizo lipo kwa nani na kuanza kupata matibabu Ili wapate mtoto inawezekana kabisa" amesisitiza.

Amesema kuwa baadhi ya chanzo Cha matatizo ya Uzazi ni pamoja na matumizi mabaya ya taulo za kike( Pads) ambapo zimekua na bakteria wanaochangia matatizo ya Uzazi,kutumia kwa wingi vyakula vya viwandani,pamoja na matumizi mabaya ya dawa, hivyo wananchi wanapaswa kujiepusha na hali hiyo .


" Twende edeni tutumie vyakula vya asili, ambapo vingine tunauwezo wa kuvilima sisi wenyewe,kwahiyo ukianza kuona dalili za kupata maumivi ya tumbo chini ya kitovu,au maumivu ya tumbo na mgongo unapaswa kwenda kumuona daktari upatiwe vipimo ili kujua kama ni tatizo la uzazi na unaweza kuja kwenye kituo chetu cha NYASOSI ili upate matibabu upone kabisa na uweze kupata mtoto bila shida yoyote" amesema

Katika hatua nyingine tabibu huyo amesema kuwa  Wanaume wengi wamekua wakisumbuliwa na ugonjwa wa tezi dume kuazia umri wa miaka 40 na kiendelea kutokana na kiungo ambacho kipo chini ya kibofu cha mkojo kupata uvimbe hivyo hali hiyo imekuwa ikiwasumbua Wanaume wengi bila kua na uelimu ya  kutosha.

Amesema kuwa tezi dume hiyo inakua inatanuka kulingana na umri wa mwanaume nakwambia endapo ikipata jeraha wakati wa kutanuka ndipo inaposababisha matatizo kutokea ikiwemo kukojoa mara kwa mara nyakati za usiku kutokana na mshipa wa kibofu kubanwa inaweza kusababisha pia saratani ya kibofu Cha mkojo.

"Mwanaume ukianza kuona dalili ya tumbo kujaa gesi na kuunguruma,au kupungua kwa nguvu za kufanya tendo la ndoa,unatakiwa kuangalia wataalamu hivyo zingatia sana hizi dalili Ili usikae muda mrefu mpaka tatizo liwe kubwa" amesema Tabibu Maduhu.

" Nakuongeza sisi hapa tuna dawa zilizothibitishwa na serikali,tuna dawa inaitwa Ntundwa ambayo inatibu tezi dume kwa muda wa  siku Saba tu unapona kabisa,hivyo wale wenye matatizo ya ugonjwa huu wafike hapa ofisini kwetu au watutafute kwa mawasiliano yetu 0788330105 tunaweza kuwapatia mahali popote walipo



Hakuna maoni