Zinazobamba

GLOBAL EDUCATION LINK KUENDELEA KUTATUA CHANGAMO ZA UPATIKANAJI WA NAFASI ZA MASOMO KATIKA VYUO VIKUU

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  Abdulmalik Mollel akizungumza na waandishi wa habari



Na Mussa Augustine.

Kampuni ya Uwakala wa Kimataifa wa kushauri na kudahili Wanafunzi kwa ajili ya kusoma Elimu ya Juu Nje ya Nchi  ya  Globala Education Link imesema kuwa itaendelea kushirikiana na Serikali katika kutatua changamoto za upatikanaji wa nafasi za masomo katika Vyuo Vikuu ndani na nje ya nchi.

Hayo yamesemwa leo Julai 22,2013 Jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo Abdulmalik Mollel wakati akizungumza na Waandsishi wa habari baada ya  kuhitimishwa kwa Maonyesho ya 18 ya Elumu ya Juu ya Sayansi na Teknolojia yaliyofanyika kuanzia Julai 17 mwaka huu chi ya Tume ya Vyuo Vikuu Nchini(TCU)

Aidha Mollel amesema kuwa tangu Maonyesho hayo yaanze yamekuwa na mwitikio Mkubwa ambapo wamefanikiwa kufanya udahili kwa wanafunzi wengi ukilinganisha na maonyesho ya miaka iliyopita.

Aidha amebainisha kuwa pamoja na kuhitimishwa kwa maonyesho hayo katika viweanja vya Mnazi Mmoja lakini Kampuni ya Global Education Link itaendlea kufanya udahili kwa wanafuzni ambao wameshindwa kufika katika viwanja vya mnazi mmoja.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  Abdulmalik Mollel akizungumza na waandishi wa habari

“Sisi kama Global Education Link tutaendlea na udahili katika ofisi zetu zilizobo barabara ya Nyerere ,hivyo wale wote ambao hawakufanikiwa kufika katika maonyesho ya Mnazi Mmoja wanaweza kufika pale ofisini nakupata huduma kuanzia jumatatu ya tarehe 24 mwaka huu”Amesema Mollel

Nakuongeza kuwa udahili huu utaendelea hadi tarehe nane siku ya nane,lengo letu ni kusaidia wale ambao hawajapata udahili wa Masomo ya Elimu ya Juu katika Vyuo vikuu vya ndani na nje ya Nchi.

Katika hatua Nyingine Abdulmalik amesema kuwa Kampuni yake imefanikiwa kufanya udahili wa wanafunzi wapatao 43 wa kitazania ambao hawakufanikiwa kumaliza masomo nchini Sudani kutokana na Machafuko ya Vita yanayoendelea.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni  Abdulmalik Mollel akizungumza na waandishi wa habari

“Hawa wanafunzi wamepata katika vyuo Vikuu Vya Nje ikiwemo India,Uturuki,Cyprus ,Malaysia hivyo ni jambo zuri ambalo limetupa faraja kuona tumewasaidia wanavyuo hawa  wengine walikua mwaka wa 2 na mwaka wa 3  chini Sudani,waweze kumaliza masomo yao”amesema Mollel

Pia ameongeza  kuwa Wanafunzi wapatao 193 ambao ni raia wa Sudani wamejiandikisha ili wafanyiwe udahili wa nafasi za masomo katika Vyuo Vikuu ndani na nje ya Nchi tunavyoshirikiana navyo ,hali ambayo ni mafanikio makubwa tuliyoyapata .

Hakuna maoni