Zinazobamba

GLOBAL EDUCATION LINK YAWAHAKIKISHIA KUPATA VYUO VIKUU WANAFUNZI WALIOSHINDWA KUENDELEA NA MASOMO SUDANI KWASABABU YA VITA

Na Mussa Augustine.

 Wanafunzi waliokwama kimasomo Nchini Sudan kutokana na machafuko na vita vinavyoendelea nchini humo,wametakiwa kuitumia Global Education Link kuwaunganisha na Vyuo Vikuu vingine ndani na Nje ya Nchi ili wasipoteze Muda muda mwingi kusubiria kumalizika kwa machafuko hayo na hata kupoteza dira ya masomo yao.

 Wito huo umetolewa Julai 18 2023 na Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link Abdulmalik Mollel wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika Banda lao lililopo kwenye maonyesho ya 18 ya Elimu ya Juu Sayansi na Teknolojia yanayoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) Ambayo yanaendelea katika viwanja vya mnazi mmoja Jiji Dar es ambayo yameanza July 17 na kutarajiwa kutamatika July 22 mwaka huu 2023.

 Abdulmalik Amesema upatikanaji wa Chuo Kikuu Bora Cha kujiunga kuendelea na mwaka wa masomo katika ya Muhula ama kuendelea na mwaka wapili au zaidi ni changamoto Duniani kote.

 "Tumeona hivi karibuni Vijana wetu wa kitanzania wamekwama katika vita na inawezekana kati yao bado wapo Tanzania,na inawezekana bado hawajabahatika kupata Vyuo Vikuu vya kuhamia,unajua Kujiunga na Chuo Kikuu sio tatizo ila kupata Chuo kinachokuruhusu wewe Mwanafunzi ma mwaka wa pili kwenda watatu ili usipoteze kile ulichokuwa umeanza kukisoma,upatikanaji Wa Vyuo Vikuu hivyo Duniani kote huwa ni tatizo"

 "Mwanafunzi huyo aliyekwama asiamini amekwama, Vyuo Vikuu Vya Ndani vyenye uwezo wa kuwachukua viwachukue,na Vyuo Vikuu vya Nje ninawahakikishia njooni kwenye maonyesho haya ya TCU ndiko platform pekee,Usiendelee kupoteza miaka yako minne ama Miwili au mitatu ya udaktari, engineering,Ama biashara ama ni Kozi yoyote ile uliyokuwa Sudan,alafu hujui sudani vita itaisha lini"

 "Maadamu Taasisi ya Elimu ya Vyuo Vikuu Nje ya Nchi Global link ipo katika maonyesho haya wewe mwanafunzi ambaye umetoka huko upo,inawezekana ukawa huna matokeo yako yote kwasababu kwenye vita kuna shida,inawezekana vyeti vyako umeviacha huko Sudan sasa anayeweza kukuelewa kirahisi ni mimi Mtanzania ndie ninaweza nikajua nifanye nini ili nihakikishe unapata chuo kingine".

 Aidha amebainisha kuwa Wanafunzi wote watakao fika kwenye maonyesho hayo na kutembelea Banda la Global Education Link Wataweza kuunganishwa kwa haraka na Vyuo Vikuu vingine vya Nje na kwa gharama ileile ya Chuo walichotoka.

"Mkikanyaga katika maonyesho haya kwenye Banda la Global Education Link mwanafunzi uliyotoka uliyekwama umetoka Sudan na unatamani kuunga Elimu yako Nje ya Nchi na kwa gharama ileile wewe njoo kuanzia kesho nielezee nikithibitisha umekidhi vigezo vya kusoma Chuo Kikuu ni jukumu langu pamoja na wewe kuwasiliana nachuo chako cha Sudan kwasababu wanawasiliana sio kwamba hawawasiliani tutapa recommendation latter na wakishindwa kutupatia tutaweka Guarantee kama Global Education Link kwa partners wetu ili kuhakikisha mtanzania hawezi kupoteza Elimu yake"

Pia amewahakikisha wale wote watakaofika Global Link kuhudumiwa na kupatiwa Chuo Kikuu wanachokihitaji ndani ya Masaa 72 pekee na kwawale wenye changamoto ya kifedha wafike watapatiwa mikopo isiyokuwa na riba kutoka katika Benki washirika.


Hakuna maoni