Zinazobamba

WAZIRI BITEKO :SERIKALI INAONDOA CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI WACHIMBAJI WA MADINI


Na Mussa Augustine.

Waziri Wa Madini Doto Biteko amewahakikishia Wachimbaji wa Madini kwamba serikali ya awamu ya sita inaipa msukumo mkubwa sekta ya Madini hivyo itahakikisha inaondoa changamoto ambazo zinawafanya washindwe kufanya shughuli zao kwa urahisi.

 Akizungumza leo Julai 19 2023 jijini Dar es salaam katika Mkutano wa  Wachimbaji wakubwa wa Madini Nchini kupitia Chama Cha Wachimba Madini Tanzania( Tanzania Chamber Of Mines) ,Waziri Biteko amesema kwamba maeneo ambayo yatafanyiwa kazi ni pamoja na Miundombinu ya Umeme na Barabara zinazoelekea kwenye Migodi.

 " Leo tumeamua kufanya Mkutano nao ili kujadili changamoto na kuwambia kitu gani serikali imekusudia kukifanya kutoka kwao,ambapo moja ya Changamoto ni Changamoto za Kodi,Kiusimamizi na tulipomaliza bunge la bajeti baada ya serikali kupitisha Muswada wa fedha( financal bill)  mambo mengi yameweza kutatuliwa" amesema Biteko.

 Aidha amendelea kufafanua kuwa katika kipindi ambacho serikali imeweka msumkumo mkubwa katika maeneo ya miundombinu ya uzalishaji ,hivyo katika fedha zote zilizotengwa kwa ajili ya umeme vijijini na mahali pengine karibu asilimia 20 ya fedha hizo zimekwenda kwenye maeneo ya migodi ya wachimbaji wakubwa,wakati na wadogo.

 Aidha amesema kuwa Wizara yake inamshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Kwa jambo hilo nakwamba mengi umeme utapelekwa kwa kiasi kikubwa katika maeno ya Migodi.

 Aidha ametaja changamoto ya Sheria nyingine kuingiliana katika maeneo ya hifadhi na Migodi,ambapo amewahakikishia wananchi kuwa serikali na maelekezo ya Rais hasa baada tu yakukutana katika semina elekezi iliyofanyika Jijini Arusha hivi karibu Rais Dkt aliagiza Wizara ya Madini kukutana na Wizara ya Maliasili na Utalii kumaliza changamoto hoyo.

 " Tutayafanyia kazi kubwa sana matatizo ambayo wachimbaji wetu wanayapata hasa katika maeneo ya hifadhi,mosi lazima tulinde hifadhi zetu lakini pia mahali penye leseni lazima pachimbwe kwa kuzingatia taratibu na sheria ambazo tunazo" amesema Waziri Biteko.

 Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tanzania Chamber of Mines,Mhandisi Filbert Rweyemamu amesema kuwa chemba ili iweze kufanya shughuli zake kwa ufanisi ni lazima kuwepo kwa mahusiano mazuri kati ya Mkusanyiko wa hiari wa watafiti,wachimbaji na watoa huduma katika sekta ya Madini.

 "Mkutano wa leo ambao tumekua tukifanya kila robo mwaka tumejaribu kutoa taarifa muhimu za maendeleo ya shughuli zetu pamoja na kueleza umma na kuiambia serikali vitu gani ambavyo vinaweza kurahisisha shughuli zetu za uzalishaji wa madini" amesema Mhandisi Rweyemamu

 Nakuongeza kuwa," tunategemea sana kama ilivyoaksiwa ifikapo mwaka 2025 sekta ya Madini iweze kuchangia angalau asilimia 10 ya pato la Taifa.

 Nae Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Faru Ghraphite ambayo inatarajia kuanza kuchimba Madini hayo Katika Mgodi wa Mahenge ,Alimiya Othman  amesma kwamba Wizara ya Fedha na Benki Kuu ya Tanzania( BOT) wameweza kutafuta masuluhisho mbalimbali katika kutatua changamoto za kifedha kwani wao ndio Wadau wakubwa katika Mradi huo. 

" Kwa kiasi fulani tumepata mafanikio mazuri,mpaka leo tulipo angalau bado kuna mambo mawili,matatu ambayo yanatakiwa kutolewa ufafanuzi katika sheria hii ya fedha ya mwaka 2023 iloyotolewa hivi karibuni.

 Amesema changamoto nyingine ni Kukosekana kwa nishati ya umeme wa uhakika kwenye Migodi lakini changamoto ambayo inapatiwa suluhisho kwasababu tupo katika mazungumzo mazuri na TANESCO na wanapata ushirikiano mzuri.

 

Halikadhalika Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Tembo Nickel Benedick Masunzu amesema kwamba katika Mradi wao wa uchimbaji wa Madini aina ya Nickel fedha ni muhimu zaidi nakwamba tayari kampuni hiyo imefanikiwa kupata kiasi cha fedha kitakachosaidia kuanza uzalishaji wa madini hayo ifikapo mwaka 2026.

 

 

Hakuna maoni