Zinazobamba

UAR YAISHAURI SERIKALI KUTOA MIKOPO SAWASAWA KWA WANAFUNZI WANAOSOMA NDANI NA NJE YA TANZANIA

Mkurugenzi wa Taasisi inayowakilisha Vyuo Vikuu Vya Nche Tanzania( UAR ) Tony Kabetha.

Na Mussa Augustine.

Serikali imeshauriwa kutoa mikopo sawasawa na Wale wanaoenda kusoma nje ya nchi ili kuwawezesha kufikia malengo yao ya kielimu pamoja na kuweza kuijenga uchumi wa Nchi .

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Taasisi inayowakilisha Vyuo Vikuu Vya Nche Tanzania( UAR ) Tony Kabetha wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya 18 ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia yaliyoandaliwa na Tume ya Vyuo Vikuu Nchini( TCU)  ambapo yanafanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es salaam.

Aidha Kabetha amesema kwamba Wanafunzi wangi wamekua na kiu ya kwenda kusoma katika vyo vya nje lakini wanashindwa kutokana na gharama ya ada kuwa kubwa hivyo serikali iweze kuwapa mikopo inayolingana na wanafunzi wanaosoma hapa nchini ili waweze kwenda kusoma na kuweza kuja kuijenga nchi kiuchumi.

“Tanzania ni nchi inayoendelea hivyo inahitaji wawekezaji wengi wa tenkolojia,tunakaribisha wawekezaji ambao unakuta wamesoma kwenye vyuo hivihivi ambavyo vijana wa kitanzania wanaenda kusoma ,naomba niishuri serikali ione namna ya kuwapatia Mikopo vijana wanaoenda kusoma vyuo vikuu vya nje.” Amesema Kibetha 

 Nakuongeza kuwa sisi kama UAR  tumekua tukiyashiriki Maonyesho haya kwa muda wa miaka zaidi ya 10 kutokana na ndoto au matarajio au mahitaji,hivyo imekua sehemu   ya vijana wengi yakuweza kujua kujua wapi waende wakasome.

Amesema kuwa changamoto kubwa iliyopo watu hawakujua nini cha kusoma hivyo walisoma vitu ambavyo leo havina soko nakwamba wamekuwa wakiwashauri  vijana yale waliyoyasoma kwa kuzingatia matakwa au sheria ya TCU kwamba yanakubalika katika nakwamba Tanzania  imefanikiwa.

Aidha ameendelea kusema kuwa Changamoto nyingine ni gharama ya kulipia ada kwenye vyuo vya nje  lakini UAR imefanikiwa kuleta  vyuo ambavyo vinatoa ufadhili  ( scholarship) ambapo ukienda kulipa ada ni sawasawa na vyuo vikuu  vya hapa Tanzania


Jengo la Mlimani Tower lililopo Mlimani City Jijini Dar es salaam ambapo ofisi za UAR zinapopatikana.

“ Kikubwa ambacho tupo nacho sisi kwa awamu hii ya tatu ni kwamba nikuhakikisha wanafunzi wanaenda kusoma kwenye vyuo na nchi  ambazo anaweza kufanya kazi na  kupata kipato  ambacho anaweza kujisaidia hata kwa ada,nchi hizo ni Marekani,Ujerumani ,Poland pamoja na Hisapania.

 Aidha amesema kuwa mbali na hilo pia vijana wengi wana vipaji mbalimbali kulingana na uwezo wao,hivyo taasisi hiyo imepata nafasi katika nchi za Ujerumani na Hispania kuwapeleka vijana wenye vipaji ili kuendeleza vipaji vyao

Amesema kuwa  UAR ni taasisi ya kwanza kutoka hapa Tanzania kwa kuweza kusaidia vijana kusoma na kupata ajira nje ya nchi.

“Malaysia na China zilikua pamoja nasi katika miaka ya sabini lakini walifanya upendeleo kwa watu wao   kwenda kusoma nje ya nchi ili waweze kufanya kazi kutokana na  ile tknoloji waliyopata kutoka nje” amesema.

 

Hakuna maoni