GLOBAL EDUCATION LINK MWAROBAINI WA TATIZO LA UPATIKANAJI WA VYUO VIKUU BORA DUNIANI
Global Education Link imewaomba Wanafunzi wa ngazi Mbalimbali za Elimu ya Juu kutembelea katika Banda lao lililopo kwenye Maonyesho ya 18 ya vyuo vikuu nchini yanayoendelea katika viwanja vya Mnazi Mmoja Jiji Dar es salaam ili kupata nafasi yakuunganishwa na Vyuo Vikuu mbalimbali Duniani.
Ombi hilo
limetolewa Julai 18 ,2023 Jijini Dar es salaam na Mkurugezni Mtendaji wa Global
Education Link Abdulmalik Mollel wakati akizungumza na Waandishi wa habari
katika Maonyesho ya 18 ya Juu,Sayansi na Teknolojia yalioyoandaliwa na Tume ya
Vyuo Vikuu Nchini(TCU) Chini ya Wizara ya
Elimu ,Sayansi na Teknoloji.
Mkurugenzi
huyo Mtendaji wa Global Education Link amesema
kuwa Wanafunzi na Taasisi zinazofadhili
Wanafunzi wafike katika banda hilo ili waweze kuunganishwa na Vyuo Vikuu vyenye ubora na
gharama nafuu.
"Wapo wanafunzi pia zipo Taasisi zinatamani
kuwafadhili wanafunzi wa Tanzania, zinatamani kupata Vyuo Vikuu ambavyo ni himilivu(affordable
)na hawajui watavipata wapi,wako wafanyakazi ambao wako maofisini wanahitaji
kujiendekeza na Elimu ya juu lakini hawawezi kusafiri,wako wa wahadhiri wa Vyuo
Vikuu wanahitaji kuongeza maarifa yao kwenye upande PHD ama Master's ,waje
kwenye Vyuo Vikuu vya Milioni 3,4 hadi 5 ambavyo nivya gharama nafuu lakini
vyenye ubora wa Elimu ya hali ya juu. Amesema Mollel.
Aidha
ameviomba Vyuo Vikuu vya Tanzania ambavyo vinahitaji ushirikiano na Vyuo Vikuu Vya
Nje kwa kufanya kazi kwa pamoja,viwasiliane wawasiliane Global Education link
ilikuweza kuungushwa na Vyuo hivyo moja kwa moja.
Mkurugezni Mtendaji wa Global Education Link Abdulmalik Mollel
"Ikiwa
kuna Chuo kitahitaji kupata Ushirikiano na Vyuo Vikuu vya Nje labda kuanza
kufundisha Mitaala yetu ya
Tanzania katika Vyuo vya Nje ama kuwakaribisha wenzetu kufanya kazi na
Vyuo Vikuu vya Ndani waelewe kwamba Vyuo Vikuu 16 kutoka katika Nchi Nane Dunia
vipo hapa kwenye mabanda ya Global Education Link,Jukumu langu kama Mtanzania
ni kusimamia Vyuo Vikuu vya Ndani na
Nje ili visaini makubaliano kwamaana MOU
yenye tija". Amesema Mollel.
Hata hivyo
Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknoloji Adolf Mkenda wakati akifungua Maonyesho
hayo Julai 18,2023 katika Viwanja Vya ,Mnazi Mmoja ameipongeza Global Education
Link kwa jitihada kubwa ya kuiunga Mkono Serikali katika kuhakikisha Wanafunzi
wanapata Elimu Bora katika Vyuo Vikuu Vya Ndani na Nje.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni