Zinazobamba

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA NCHINI JAJI FRANCIS MUTUNGI AWATAKA WANASIASA KUFANYA SIASA ZA KISTAARABU

        Msajili wa Vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi

Na Mussa Augustine

Msajili wa Vyama vya siasa Jaji Francis Mutungi ametoa wito kwa vyama vya siasa kufanya siasa zenye ustaarabu na zinazozingatia Sheria ili kuendelea kulinda Amani ,Utulivu pamoja na Umoja.

Hayo ameyasema Agost mosi ,2023 wakati wa Mkutano wa Baraza la Vyama vya siasa lililowakutanisha viongozi wa dini na vyama vya siasa likiwa na malengo ya kuelimishana namna ya kufanya siasa safi zitakazolinda utu na Taifa kwa ujumla.

Aidha amesema kwamba Baraza la Vyama vya siasa limekua likifuatilia mwenendo wa siasa zinazoendelea hapa nchini,nakwamba limeona liwakutanishe viongozi wa kisisasa pamoja  na viongozi wa dini ili kuelimishina jinsi ya kufanya siasa kwa kuzingatia mipaka ya kazi  za siasa na dini.

"Leo tumekutana na  viongozi wa dini na viongozi wa siasa kwani tumekua tukifuatilia siasa zinazoendelea hapa nchini tumeona sio nzuri kwani kumekuwa na matumizi  lugha za matusi na kukejeli,pia viongozi wa dini kuhusishwa kwenye siasa hizo." amesema Msajili huyo wa Vyama vya Siasa Nchini.

 Nakuongeza kuongeza kuwa mazingira mazuri aliyoyaweka na Rais Samia katika kufanya siasa yanapaswa yatumike vizuri ili kuboresha siasa nchini nakuachana na siasa za kushambulia viongozi kwa matusi,kutoa lugha za udhalilishaji wa kijinsia,kuacha kutumia vikundi kuhamasisha vurugu na uvunjifu wa Amani.

Nae Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Alexander Makulilo  amesema kuwa uhusiano wa siasa na dini ni changamano hivyo serikali inapaswa kuweka Sheria ili kudhibiti  Muungano huo, nakwamba  sheria zimekataza kutumia viongozi wa dini katika Majukwaa ya Siasa wakati wa kunadi sera za vyama vyama vya siasa..

Makulilo amesisitiza kuwa Matumizi ya lugha za uchochezi, kudharirisha nchi, lugha za kibaguzi, lugha za udharirishaji wa jinsia zimepigwa marufuku  badala yake vyama vya siasa vinapaswa kuuza  sera zao ili waungwe mkono.

Aidha ameendlea kusema kuwa  Sheria hairuhusu chama chochote Cha siasa kuwa na walinzi wa viongozi na Mali za chama badala yake kazi hiyo ni ya jeshi la polisi.

Kwa upande wake mwanasiasa Mkongwe John Cheyo amewaomba wanasiasa nchini kuwa wazalendo kwa nchi yao kwa kufanya siasa zisizodhalilisha  nchi wala kumtukana Rais na kiongozi yeyote wa serikali na chama,nakwamba waendelee kudumisha tunu za Taifa ambazo ni Umoja,Amani na Mshikamano.

"Ni aibu kwa kiongozi wa siasa kusimama jukwaani na kuanza kuisema nchini yako na viongozi wako hiyo sio siasa ambayo inapaswa kuwepo huo sio uzalendo, tunapaswa kuwa wazalendo kwanza kwa nchi yetu." amesema mwenyekiti huyo Taifa wa UDP Jonh Cheyo

Naye Padri Frolence Lutaiwa kutoka Baraza la maaskofu (TEC) amesema viongozi wa dini wanapaswa kukemea maovu na si kushiriki katika uovu hivyo viongozi wa dini wanapaswa kuwa mstari wa mbele kuwaasa wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu zenye kujenga umoja, amani na mshikamano wa Taifa

Kwa upande wake Mwenyekiti wa jumuiya na Taasisi za kiislam nchini shekh Musa Kundecha amesema ni ngumu kutenganisha dini na siasa hivyo viongozi wanapaswa kutumia majukwaa ya siasa kutangaza amani na imani  ili kufanya wananchi kuwa na hofu ya Mungu na si kuwabagua kutokana na uchama au udini.

Hata hivyo baadhi ya Viongozi wa Vyama vya siasa akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Democrat Party (DP) Abdul Mluya wamesema kuwa mkutano huo umewasaidia kuwakumbusha mambo mengi nakwamba yale yote waliyoelekezwa watayazingatia katika kudumisha Amani na Utulivu kwa Taifa.

Hakuna maoni