Zinazobamba

Waziri Ummy : Hali ya Maambukizi Mapya ya UVIKO 19 Nchini Tanzania na Duniani Kote Yamepungua.

                         Waziri wa Afya Ummy Mwalimu

Na Mussa Augustine.

 Serikali ya Tanzania imepunguza Masharti ya kujikinga na Ugonjwa wa Uviko 19 ikwemo kuondoa  ulazima wa kuvaa barakoa isipokuwa pale inapobidi, baada ya nchi kufikia asilimia 60 ya walengwa wa chanjo ya Uviko19.

Akizungumza na Waandishi wa habari  Jijini Dar es salaam  Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema licha kupunguzwa kwa masharti hayo Serikali inahimiza Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari ya Ugonjwa wa Uviko 19 kunawa mikono Kwa maji tiririka na sabuni kutumia vipukusi kujikinga na magonjwa mengine ya kuambukiza  ikiwemo kuhara,kipindupindu.

 "Toka kutangaza kwa uwepo wa Uviko-19 nchini mwezi Machi 2020 mpaka kufikia 7Septemba 2022 Tanzania tumeshuhudia jumla ya visa 35,747 vilivyothibitishwa  vya maambukizi ya Uvico-19 na vifaa 808"amesema Waziri Ummy

 Hata hivyo uchambuzi katika Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii na vituo vya kutolea huduma za afya septemba 7 2022 imeonesha kuwa kati ya watu 289  waliopimwa watu 23 wamethibitishwa kuwa na maambukizi ya Uviko-19 huku wagonjwa 7 walilazwa wodini na wote hawajapata chanjo ya ugonjwa huo na mgonjwa mmoja anatumia hewa tiba ya Oksijeni hivyo ugonjwa bado nchini .

 "Serikali inaendelea kufanya uchunguzi wa afya dhidi ya magonjwa ya milipuko kwa wasafiri wa kimataifa katika Viwanja vya ndege vya kimataifa,bandarini na mipaka ya nchi kavu kufanya vipimo vya vipima joto (thermoscans) huku kusitisha kufanya kipimo cha haraka (Rapid Test) kwa wasafiri wanaotoka nchi zote wenye vyeti vya chanjo Uviko-19 au cheti Cha TT-PCR " amesema

 Hata hivyo pamoja na hayo amesema Serikali imeongeza umri wa watoto kutoka nje ya nchi wanayotakiwa kusamehewa kupima Uviko-19 kabla hawajaingia nchini kutoka umri wa miaka 5 ilivyokuwa awali  Hadi miaka 12.

 Aidha Waziri huyo wa afya amewashukuru waandishi wa habari pamoja na wadau wa Maendeleo wakiwemo  WHO,UNICEF,USAID,CDC,GAV na mashirika yasiyo ya kiserikali kwa mchango wake mkubwa wa mapambano dhidi ya Uviko-19.

 

Hakuna maoni