Ukweli kuhusu kitabu cha sheikh Ponda huu hapa, achambua Mbivu, mbichi
Na Suleiman Magali
Ikiwa imebaki siku mbili kitabu cha Juhudi na
Changamoto kilichoandikwa na Sheikh Ponda Issa Ponda kuzinduliwa, Mwenyekiti
ambaye anaratibu kongamano la uzinduzi wa kitabu hicho amefichua kuwa kitabu
hicho kimejaa ukweli na uhakika huku
rejea na data zilizotumika zikiwa za kuaminika.
Pia alisema, kitabu hicho kinachosubiriwa kwa
hamu na watanzania waliopo ndani na nje ya nchi kimepata mwitikio mkubwa kutoka
kwa wadau licha ya kwamba bado hakijazinduliwa.
Akizungumza na gazeti imaani, Mwenyekiti huyo,
Bw. Ibrahim Zuberi Mkondo alisema kitabu kimepata mwitikio mkubwa
baada ya watu kupiga simu kwa wingi wakikiulizia licha ya kwamba bado
hakizazinduliwa.
Aidha kuhusu maandalizi tayari yameshakamilika na zoezi lililobaki
ni kuzinduliwa siku ya Jumapili, katika ukumbi wa Peacok Hotel, Dar es Salaam.
Pia akizungumzia kuhusu kitabu hicho, Mkondo alisema Kitabu
kimeeleza mambo mengi na mazuri, kimeeleza juhudi za waislam kabla na baada ya
uhuru na changamoto ambazo waislam wamekuwa wakipitia katika kila hatua.
“Tunapoeleza juhudi na changamoto maana yake waislam na wasio
waislam watasoma walichokifanya viongozi/masheikh toka enzi hizo, watapitishwa
kwenye mipango na mikakati ambayo imekuwa ikifanyika katika kuleta mabadiriko
kwenye jamii ya kiislam,” alisema
Tunapoeleza changamoto watu wafahamu, kuwa tumejadiri kwa kina
changamoto ambazo waislam wamepitia katika kila zama, lengo ni kuwafanya watu
wasirudi nyuma.
Tunataka kuona wanapojaribu kuliendea jambo wafahamu kuwa linaweza
kuwa na changamoto zake na wanapaswa kujiandaa nazo ili kuzishinda na kupata
mafanikio.
Alisema Matarajio makubwa kwa umma ni kupata elimu iliyopo ndani
ya kitabu, nachotaka kuwaambia wasomaji wanapaswa wajiandae, kitabu kina vitu
vingi vipya ambavyo watu bado hawajawahi kupata kusoma au kuhadithiwa.
Utakumbuka kuwa waandishi wengi wa vitabu wamekuwa wakitazama vitu
ambavyo haviwezi leta athari kubwa katika kazi zao, lakini kwa Sheikh Ponda
hana woga huo, ni mtu ambaye hajawahi kurudi nyuma katika jambo analolisimamia,
hivyo hata kwenye uandishi wa kitabu hiki ameandiika vitu vya kweli hata kama
vinaumiza.
Watu watarajie vitu muhimu ambavyo vinaweza saidia katika historia
ya harakati za waislam na jamii kwa ujumla, ndani ya nchi na nje ya nchi
Aidha kuhusu ushauri wangu kwa jamii ni kwamba niwaombe wafanye
jitihada za kupata kopi ya kitabu hiki cha Juhudi na changamoto, ni kitabu
ambacho hutajutia kukisoma, kimejaa mambo mazuri na hakichoshi katika usomaji
wake.
Mbali na kutoa wito kwa jamii kukisoma kitabu cha Sheikh Ponda,
pia amewakumbusha masheikh na viongozi wa kada mbalimbalin kujenga utamaduni wa
kuandika vitabu, kwani anaamini kuwa katika uongozi watu wanajifunza mambo
mengi.
“Mfano kwenye jamii ya Kiislam, watu wasingesoma historia ya
uongozi wa Mtume kama hakuna waandishi, kama maisha yake yasingeandikwa basi kuna
vitu vingi ambavyo umma usingejifunza,” alisema.
Vilevile alisema watu waandike chanya na hasi, hata kama
ikitokezea hukufanya vizuri katika eneo lake kwa sababu kadhaa ni vizuri akaziandika
na watu wakajifunza jambo hilo.
“Tunatamani kuona watu wanajifunza ili kuboresha au kuongeza
katika jambo husika, uzoefu ni mwalimu mzuri, watu wasidhani kuandika ni jukumu
la watu flani, hapana hili ni jukumu letu na tunapaswa kutoa elimu kwa vizazi
vinavyokuja” aliongeza.
Aidha akieleza jambo ambalo limemfurahisha baada ya kukiona kitabu
hiko, Mkondo alisema yapo mambo mengi yamenifurahisha lakini kubwa ni ni ukweli
usio na woga ambao Sheikh Ponda ameueleza.
Alisema Watu wengi wamekuwa na tabia ya kuandika vitabu kwa
kuvicha baadhi ya taarifa ama kuweka lugha za mafumbo kwa kuzingatia sababu
mbalimbali jambo ambalo Sheikh Ponda hakukifanya. Sheikh amekuwa mkweli na
muwazi kitu ambacho hata wasomaji wakisoma watanufaika nacho
Alisema Kitabu kina rejea za kutosha, data za kutosha, hakuna kitu
cha kubabaisha na anaamini watu wakisoma watapata elimu sahihi sio vitu ambavyo
vimetengenezwa tengenezwa.
Akieleza upatikanaji wa kitabu hicho, Mkondo alisema Vitabu
vitapatikana nchi nzima, tayari wamejipanga kuweka mfumo mzuri ili watu wengi
waweze kupata kitabu.
Sheikh Ponda Issa Ponda anatarajia kuzindua kitabu chake cha
Juhudi na Changamoto, Jumapili 4, 2022 katika ukumbi wa Peacock hotel, Jijini
Dar es salaam kuanzia majira ya saa tatu hadi kukamilika kwake saa sita
Mgeni rasmi katika kongamano hilo anatarajiwa kuwa Dkt Omar Tego,
msomi wa siku nyingi anayefanya kazi Chuo Kikuu cha Kiislam MUM
Kwa mujibu wa Sheikh Ponda, kitabu cha Juhudi na Changamoto kwa
awamu ya kwanza wanatarajia kudurufu kopi 5,000 na kusambaza katika maduka yote
ya Ibn Azim, lakini pia mikoani kutafanyika mipango ili kiwafikie kwa urahisi.
Mbali na kitabu cha Juhudi na Changamoto ambacho tayari
kimeshakamilika kwa asilimia 100, Sheikh Ponda tayari amekamilisha miswada ya vitabu
vingine 15 kwa asilimia 90 na vitaanza kuachiwa hatua kwa hatua.
Vitabu ambavyo tayari miswada yake imekamilika kwa asilimia 90% ni
pamoja na kitabu cha Wako wapi raia hawa, Pitio la Zanzibar, Matukio na Habari,
Ukweli katika utafiti wa Sivalon, Mahakama ya Kadhi Tanzania pamoja na
Kiswahili Chawekwa Rehani.
Vingine ni Hijja Kongamano la Ulimwengu, Mwembechai, Mazingatio
(Consideration), Masheikh gerezani, Ulamaa na Majukumu, Waislam na Mkono wa
Dola, Mantiki za Ndoa za Mtume, Mafunzo ya umoja na Harakati za Vijana Sita.
Sheikh alisema kitabu cha
Juhudi na Changamoto kinapatikana kwa Shilingi 15000.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni