Zinazobamba

WANAWAKE WATAKIWA KULINDA VICHANGA VYAO






Joyce Joliga Songea

Wanawake wajawazito na wanaonyonyesha wameshauriwa kuacha Mzaha na kuwakinga watoto wao kwa kufata maelekezo yanayotolewa na wataalam wa afya namna ya kujikinga na virusi vya corona ili kuweza kujikinga wao na Watoto wao wasiambukizwe kwani ugonjwa huo ni hatari na unaua.


Ushauri huo umetolewa na Mganga mfawidhi Hospitali ya Rufaa ya Songea Daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake na watoto wakati akizungumza na Mwananchi ofisini kwake jana.

Alisema, tupo katika kipindi kigumu na hivyo wazazi wanapaswa kuwalinda watoto wao wachanga na wale ambao bado ni wadogo wawaelimishe kwa kuwaeleza wasicheze sehemu zenye mikusanyiko ya watu wengi na wanawe mikono mara kwa mara na kukaa umbali wa mita moja hadi mbili ili kujilinda wasiambukizwe.

Alisema, Hospitali hiyo imeshatenga eneo maalum iwapo itatokea wagonjwa wa corona ambapo kuna eneo maalum kwa ajili ya wajawazito na wanaonyonyesha kama muongozo wa wizara ya afya unavyoelekeza ingawa hadi sasa wanashukuru Mungu hawajapata kesi yoyote kuhusiana na corona 

Alisema kutoa elimu kwa wananchi na wamepunguza misongamano isiyo muhimu ya watu kwenda kuona wagonjwa katika kipindi hiki ikiwa ni pamoja na kuchukua tahadhari kwa kuweka sanitizer maeneo yote ya Hospitali na wagonjwa kukaa mita mbili pindi wanapoenda kupata matibabu

“Wazazi tujifunze kupitia nchi za wenzetu huu ugonjwa upo na tayari umeshaingia hapa nchini ni jukumu Letu sote kufata maelekezo ya wataalam wetu kwa kunawa mikono kwa sabuni wakati wote, Tukae majumbani na kuwazuia watoto wetu kwenda kucheza kwenye watu wengi pia tuhakikishe tunapohisi dalili za kikohozi , Mafua makali, joto la mwili kupanda na kubanwa kifua tuwahi hospitali kupata matibabu ili tuweze kujilinda na kuwalinda wenzetu ,”

Aidha anawataka wananchi hasa wajawazito na wanaonyonyesha kuendelea kuhudhulia kliniki ili wapewe elimu zaidi ya kujikinga na kulinda vichanga vyao .

Hakuna maoni