ANAYETUHUMIWA "KUNUNUA MADIWANI ARUSHA"ASHINDA UCHAGUZI WA CCM,SOMA HAPO KUJUA
Arusha. Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Elexander Mnyeti ambaye anatuhumiwa na Wabunge wa Chama cha Chadema,Mkoani Arusha kuwa ndiye kinala anayenunua madiwani ili wahame chadema na kuhamia Ccm, leo amechaguliwa kuwa mmoja wa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa CCM akiwakilisha wilaya ya kichama ya CCM ya Meru.
Mnyeti katika uchaguzi huo, alishinda baada ya kupata kura 266 akiwa hayupo ukumbini.
Katika nafasi hiyo ambayo ilikuwa inagombewa na wanaCCM 22, wajumbe wengine waliochaguliwa na Mkurugenzi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha(AICC), Elishilia Kaaya aliyepata kura 258 na Dk Daniel Mirisho alipata kura 327.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, uliofanyika ukumbi wa Chuo Kikuu cha Makumira, mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake wilaya ya Arusha, Mary Kisaka amesema katika nafasi hiyo, waliopiga kura walikuwa 586 kura zilizoharibika zilikuwa 3 na kura halali 583.
Katika nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Wilaya Meru, mwenyekiti aliyemaliza muda wake, Andew Mungure aliweza kutetea kiti hicho baada ya kuwabwaga wagombea wenzake wawili.
Mungure alipata kura 471 na kuwabwaga Nevangirwa Mmari aliyepata kura 106 na Daniel Kaaya aliyepata kura 28.
Katika uchaguzi huo, Mbwana Hungura alichaguliwa kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa wilaya hiyo baada ya kupata kura 50 na kuwashinda wanaCCM wengine wane ambapo kura halali zilikuwa ni 97.