MBUNGE KUBENEA ACHARUKA ,NAIBU WA WAZIRI WA JPM KUMLIPA MAMILIONI,AIBUKA NA MZIMU WA DK ULIMBOKA,SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
WIKI moja
kupita baada ya serikali ya Rais John Magufuli kulifungia gazeti linalotoka
mola moja kwa wiki la Mwanahalisi, kwa miaka miwili kwa madai ya kuwa Gazeti
hilo linaandika habari wanazodai zinakiuka kanuni za uandishi wa habari,Wamiliki
Gazeti hilo wameibuka na kuipa siku mbili serikali kulifungulia gazeti hilo kabla
ya kwenda mahakamani.
Pia wamesema
endapo serikali ikikataa ombi lao watamfungulia binafsi kesi Naibu waziri wa
habari.sanaa,burudani na michezo ,Anastazia Wambura ya kutaka fidia ya milioni 41 ya kila chapisho
la gazeti ambalo litakuwa halitoki tangu kufungiwa kwa madai sheria haijampa mamlaka ya kulifungia gazeti.
Hayo
yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam, na mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Hali
Halisi Puplishers Limited ,Saed Kubenea wakati wa mkutano na waandishi wa habari
amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kubaini kuwepo na uonevu wakati wa kulifungia gazeti hilo.
“Tumewaandikia
barua hawa watu kuwa ndani ya siku mbili walifungulie Gazeti hili,na kama wakikaidi
mwanasheria yupo hapa tunakwenda kufungua kesi binafsi kwa Naibu waziri ,tunataka watulipe hela
hii ya milioni 41 moja ya kila toleo la
gazeti ambalo alitoki ikiwa ni hasara aliotuingizia” Amesema Kubenea.
Kubenea
ambaye ni Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) amesema hata hatua ya serikali kuliifungia gazeti la Mwanahalisi ni
kuidharau muhimili wa mahakama kutokana na Mahakama kuu kutoa umuzi wa kutoguswa gazeti hilo.
“Leo tunashangaa serikali hii inapuuza uamuzi
wa mahakama ambao ulitaka gazeti hili lisiguswe kwa namna yeyote,maana Jaji
alisema kama waziri akitaka kuligusa gazeti hili anatakiwa kwenda mahakamani na
mahakama kutoa maauzi,lakini tunashangaa leo wanakuja kulifungia gazeti”
“Na hata
ukiangalia barua ya kufungia gazeti hili,imesainiwa na Naibu waziri wakati sheria
ya Huduma ya habari ya 2016 imemtaja Waziri na sio naibu waziri,pia sheria
hiyo haimpi waziri kulifungia gazeti
bali inamtaka kuzuia tu maudhui sio kufungia gazeti”amesema Kubenea.
Naye
Mwanasheria wa Kampuni hiyo,Fredrick Kiwelo amesema kwa sasa wameshamwandikia
notsi ya siku mbili Naibu waziri kuondoa zuia la kulifungia Gazeti.
“Hawa
tumewashaaandikia barua,huku tujiandaa kwa taratibu zengine za kufungua kesi za
kudai fidia maana kumetokea ukiukwaji mkubwa kwenye kulifungia kesi’Amesema
Kiwelo.
KUHUSU TUHUMA ZA GAZETI LA MWANAHALISI
Kubenea
ambaye ni Mwandishi Nguli wa habari nchini kwa sasa, amesikitishwa na maelezo
yaliyotolewa na Mkurugenzi wa habari Maelezo,Dkt Hassan Abasi kuwa gazeti la
mwanahalisi limekuwa likiandika habari za kutunga na zenye kukiuka kanuzi na
misingi ya taaluma na habari.
Kubenea
amesema maelezo ya Mkurugenzi huyu ni ya kupuuzwa kwani gazeti lake limekuwa
likiandika habari za ukweli.
“Hili Gazeti
linaendeshwa na watu weledi kwenye vyombo vya habari si vyeti tu bali
wanauadilifu mkubwa wa kimaadili,leo miongoni mwa wahariri wa gazeti hili ni, Nyaronyo
Kichele huyu alikuwa ni mhariri wa gazeti la Kulikoni ambalo hapa Abassi
ndipo alipofanya kazi,sasa leo walimfundisha kazi huyu Abassi leo ndio
wanaandika habari za uongo?”Amehoji kubenea.
Mbunge huyu
Mchachali amesema kwa sasa kinachoisumbua serikali kwa sasa ni kutokana na wamiliki
wa gazeti hilo kukataa “kuilamba miguu serikali”
"Nataka ni waambieni tulipofungia mara ya kwanza mwaka 2012 kutokana na kuandika habari ya kutekwa,kupigwa na kutupwa kwa kiongozi wa madaktri nchini Dk Steven Ulimboka,tulimtaja mtu mmoja anaitwa Ramadhan Igondu kuwa nahusika ,na hata serikali hakuna mahala popote walipokanusha kuhusu huyu mtu na hata Dk Ulimboka alikuja na kukiri kumfahamu huyu mtu na akamtaja nahusika ,"
"Na hata tulipokwenda mahakamani serikali ikatufungulia gazeti ,sasa leo unaposema gazeti hili linaandika habari za uongo ni vipi"ameendelea kuhoji
"Na hata tulipokwenda mahakamani serikali ikatufungulia gazeti ,sasa leo unaposema gazeti hili linaandika habari za uongo ni vipi"ameendelea kuhoji