Zinazobamba

MBUNGE KUBENEA ACHARUKA ,NAIBU WA WAZIRI WA JPM KUMLIPA MAMILIONI,AIBUKA NA MZIMU WA DK ULIMBOKA,SOMA HAPO KUJUA


NA KAROLI VINSENT
WIKI moja kupita baada ya serikali ya Rais John Magufuli kulifungia gazeti linalotoka mola moja kwa wiki la Mwanahalisi, kwa miaka miwili kwa madai ya kuwa Gazeti hilo linaandika habari wanazodai zinakiuka kanuni za uandishi wa habari,Wamiliki Gazeti hilo wameibuka na kuipa siku mbili serikali kulifungulia gazeti hilo kabla ya kwenda mahakamani.
Pia wamesema endapo serikali ikikataa ombi lao watamfungulia binafsi kesi Naibu waziri wa habari.sanaa,burudani na michezo ,Anastazia Wambura  ya kutaka fidia ya milioni 41 ya kila chapisho la gazeti ambalo litakuwa halitoki tangu kufungiwa kwa madai sheria haijampa mamlaka ya kulifungia gazeti.
Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam, na mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Hali Halisi Puplishers Limited ,Saed Kubenea wakati wa mkutano na waandishi wa habari amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kubaini kuwepo na  uonevu wakati wa kulifungia gazeti hilo.

“Tumewaandikia barua hawa watu kuwa ndani ya siku mbili walifungulie Gazeti hili,na kama wakikaidi mwanasheria yupo hapa tunakwenda kufungua kesi binafsi  kwa Naibu waziri ,tunataka watulipe hela hii  ya milioni 41 moja ya kila toleo la gazeti ambalo alitoki ikiwa ni hasara aliotuingizia” Amesema Kubenea.
Kubenea ambaye ni Mbunge wa Ubungo (CHADEMA) amesema hata hatua ya  serikali kuliifungia gazeti la Mwanahalisi ni kuidharau muhimili wa mahakama kutokana na Mahakama kuu kutoa  umuzi wa kutoguswa gazeti hilo.

 “Leo tunashangaa serikali hii inapuuza uamuzi wa mahakama ambao ulitaka gazeti hili lisiguswe kwa namna yeyote,maana Jaji alisema kama waziri akitaka kuligusa gazeti hili anatakiwa kwenda mahakamani na mahakama kutoa maauzi,lakini tunashangaa leo wanakuja kulifungia gazeti”
“Na hata ukiangalia barua ya kufungia gazeti hili,imesainiwa na Naibu waziri wakati sheria ya Huduma ya habari ya 2016 imemtaja Waziri na sio naibu waziri,pia sheria hiyo  haimpi waziri kulifungia gazeti bali inamtaka kuzuia tu maudhui sio kufungia gazeti”amesema Kubenea.

Naye Mwanasheria wa Kampuni hiyo,Fredrick Kiwelo amesema kwa sasa wameshamwandikia notsi ya siku mbili Naibu waziri kuondoa zuia la kulifungia Gazeti.

“Hawa tumewashaaandikia barua,huku tujiandaa kwa taratibu zengine za kufungua kesi za kudai fidia maana kumetokea ukiukwaji mkubwa kwenye kulifungia kesi’Amesema Kiwelo.

   KUHUSU TUHUMA ZA GAZETI LA MWANAHALISI
Kubenea ambaye ni Mwandishi Nguli wa habari nchini kwa sasa, amesikitishwa na maelezo yaliyotolewa na Mkurugenzi wa habari Maelezo,Dkt Hassan Abasi kuwa gazeti la mwanahalisi limekuwa likiandika habari za kutunga na zenye kukiuka kanuzi na misingi ya taaluma na habari.

Kubenea amesema maelezo ya Mkurugenzi huyu ni ya kupuuzwa kwani gazeti lake limekuwa likiandika habari za ukweli.

“Hili Gazeti linaendeshwa na watu weledi kwenye vyombo vya habari si vyeti tu bali wanauadilifu mkubwa wa kimaadili,leo miongoni mwa wahariri wa gazeti hili ni, Nyaronyo Kichele huyu alikuwa ni mhariri wa gazeti la Kulikoni ambalo hapa Abassi ndipo alipofanya kazi,sasa leo walimfundisha kazi huyu Abassi leo ndio wanaandika habari za uongo?”Amehoji kubenea.

Mbunge huyu Mchachali amesema kwa sasa kinachoisumbua serikali kwa sasa ni kutokana na wamiliki wa gazeti hilo kukataa “kuilamba miguu serikali”

"Nataka ni waambieni tulipofungia mara ya kwanza mwaka 2012 kutokana na kuandika habari ya kutekwa,kupigwa na kutupwa kwa kiongozi wa madaktri nchini Dk Steven Ulimboka,tulimtaja mtu mmoja anaitwa Ramadhan Igondu kuwa nahusika ,na hata serikali hakuna mahala popote walipokanusha kuhusu huyu mtu na hata Dk Ulimboka alikuja na kukiri kumfahamu huyu mtu na akamtaja nahusika ,"

"Na hata tulipokwenda mahakamani serikali ikatufungulia gazeti ,sasa leo unaposema gazeti hili linaandika habari za uongo ni vipi"ameendelea kuhoji