Zinazobamba

WAZIRI UMMY MWALIMU NA WIZARA YAKE YAJITOSA KUMALIZA TATIZO LA MAGONJWA YSIYO YA KUAMBUKIZWA,SOMA HAPO KUJUA

ummy-one
Pichani ni Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu Picha na Maktaba
Katika kuhakikisha Watanzania wanakuwa na utaratibu wa kujihusisha na mazoezi ili kupunguza hatari ya kupata magonjwa ambayo sio ya kuambuza, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa kampeni ya kuhamasisha mazoezi ya AFYA YAKO, MTAJI WAKO, FANYA MAZOEZI, LINDA AFYA YAKO itakuwa endelevu na itafanyika nchi nzima.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifunga mafunzo ya siku moja kwa waandishi wa habari yaliyokuwa yanalenga kutoa elimu kwa wanahabari kuhusu magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
“Kila mwezi tutakuwa tukichagua mkoa ambao mazoezi yatakuwa yanafanyika na yatakuwa yakiongozwa na mimi, au naibu waziri au katibu mkuu naibu katibu mkuu au hata viongozi wengine na hakutakuwa na gharama maana tunajua tukianza kuweka hayo mambo kutajitokeza changamoto nyingine,” alisema Ummy.
Waziri Ummy alisema alifikia uamuzi wa kuanzisha kampeni hiyo kutokana na takwimu kuonyesha kuwepo kwa idadi kubwa ya watu ambao wamekuwa wakipoteza maisha kutokana na magonjwa yasiyo ya kuambikiza na wakati ni jambo ambalo linaweza kumalizika kama wananchi watabadili mfumo wao wa maisha na kuanza kuwa wanafanya mazoezi.
Nina mwaka hapa wizarani wakati nimefika kipaumbele changu kilikuwa ni afya ya mama na mtoto lakini kumbe tukasahau upande mwingine, ripoti inaonyesha kati ya watu 100 ambao wanapoteza maisha, 27 wanakufa kutokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, sasa niamua lazima tulishughulikie jambo hili,” alisema Waziri Ummy.
Pia aliwataka Watanzania wote kujitokeza Desemba, 17 katika viwanja vya Leaders Club kuanzia saa 12:30 asubuhi katika uzinduzi wa kampeni ya kitaifa ya kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambapo mgeni rasmi atakuwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan