MAUZO KATIKA SOKO LA HISA YAONGEZEKA MARA DUFU,SOMA HAPO KUJUA
NA KAROLI VINSENT
MAUZO katika soko la hisa la mkoa wa Dar es Salaam (DSE)yameongezeka
mara 6 kutoka milioni 198 kwa wiki iliyopita hadi kufikia Tshs.1.22 Bilioni kwa
wiki iliyoishia Desemba 9 ya mwaka huu.
Hata hivyo,Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa
kwa wiki iliypita yameongezeka kwa
asilimia 44 kutoka wa hisa 262,589 kwa wiki iliyopita hadi kufikia hisa 378,149
kwa wiki hiyo ilishoishia pia Desemab 9.
Hayo yamebainishwa leo Jijini Dar es Salaam na Afisa Mwandamizi wa mauzo wa (DSE)Marry Kinabo
wakati wa mkutano na waandishi wa habari amesema sababu iliyochangia ongezeko
hilo la mauzo imetokana na wawekezaji wengi kwenye soko kuwekeza zaidi kwenye kununua hisa na sio
kuwekeza kwenye hati fungani.
Kinabo amesema ukubwa mtaji wa soko wa makampuni kwa
ujumla umeshuka kwa asilimia 0.5 kwa makampuni ya ndani kwa kuendelea kubaki kiwango kile kile cha
trioni 8.
Ameongeza kuwa katika sekta ya viwanda imeshuka kwa
point 104.63 na sekta ya huduma za kibenki na fedha imeshuka kwa point 3.66 .
Kinabo amezitaja pia Kampuni tatu zilizoongoza idadi
kwa mauzo ni DSE kwa silimia 47,Benki ya DCB kwa silimia 19 pamoja na kiwanda
cha TBL kwa silimia 18