Zinazobamba

UTAWALA WA MAGUFULI WAKOSOLEWA VIBAYA,CHAMA CHA NCCR MAGEUZI CHAUVAA UTUMBUAJI WAKE MAJIPU,SOMA HAPO KUJUA


Pichani aliyeshika kitabu Chekundu ni miongoni mwa watendaji walioamuliwa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda kukamatwa kwa madai ya kuuza viwanja vya wananchi
Chama cha Nccr Mageuzi  kimeukosoa vikali mwenendo wa utawala wa Rais John Magufuli hatua yake ya kuwasimasha au kuwafukuza kazi watendaji wa serikali ambayo imebeba jina la (Utumbuaji majipu),huku chama hicho kikidai hatua hiyo imezidisha uoga kwa watumishi na kuchangia kuzoletesha uwajibikaji,Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Kauli hiyo ya Nccr mageuzi inakuja ikiwa ni siku moja kupita baada Chama cha wafanyakazi nchini (TUCTA) kumlalamikia waziri mkuu hatua hiyo kwa kusema inakwenda kinyume na sheria za kazi na ajira.


Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam katibu mkuu wa  Nccr Juju Banda amesema kitendo cha mawaziri, wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya kuwafukuza watendaji wa serikali bila hata kufanya uchunguzi kinakwenda kinyume na sheria za kazi na kuleta uoga kwa watumishi.

Amesema Chama hicho,hakipingi uchukuaji wa  hatua kwa watu wanaofanya ubadilifu wa mali za umma bali wanapinga hatua ya inayochukiwa sasa watendaji kwa kile alichodai watumishi wengi wamekuwa wakifukuzwa kazi bila hata uchunguzi kufanyika,


“Leo hali ya nchi ni mbaya,watumishi wa umma wanafanya kazi kwa uoga huku wakimuogopa mkuu wa wilaya au mkuu wa mkoa,kwani wamekuwa wakifika sehemu za kazi na kuamulu watumishi wa umma kukamatwa au kufukuzwa kazi bila hata ya uchunguzi kufanyika,na hii hatua imepeleka watumishi wa umma kufanya kazi kwa uoga na hali hii itapeleka maendelea kuchelewa”amesema Banda.

Hata hivyo,Banda ametabili uwenda serikali ikaingia kwenye hasara kubwa ya kuwalipa watumishi hao ambao inawafukuzwa kwa kile alichodai watumishi hao wakiamua kwenda kwenye vyombo vya  mahakama wakipinga kufukuzwa wao kazi ambapo kumejaa uonevu na kupelea mahakama kutoa haki ya wafanyakazi hao.

Katika Hatua nyingine Chama hicho kimetanga kuanza ziara nchi nzima yenye lengo la kukijenga chama hicho kueleka kwenye chaguzi zinazokuja mbeleni.