Zinazobamba

SAKATA LA KATIBA MPYA: JUKWAA LA KATIBA WAMNG'ANG'ANIA RAIS MAGUFULI, WASEMA KAMA YEYE HAJASEMA LAKINI CHAMA CHAKE KIMESEMA


Mratibu wa Jukwa la katiba Tanzania JUKATA Ndugu Hebron Mwakagenda Pamoja na Viongozi wengine wa mashirika yanayoshirikiana na Jukata wakionyesha Kitabu maalum ambacho kimezinduliwa Leo kwa ajili ya kuhamasisha Upatikanaji wa katiba moya baada ya mchakato huo kukwama kusikujulikana.Kitabu hicho kinaeleza Mwelekeo wa katiba Mpya Tanzania,Tulikotoka,Tulipo,na Tuendeko(Picha na Exaud Mtei)
Jukwaa la katiba Tanzania (JUKATA) Rais Magufuli hawezi kukwepa kuhusu suala la kupatikana kwa katiba mpya kwani yeye si Rais wa mgombea huru bali amepelekwa na chama ambacho kimewaahidi watanzania kuwa katiba mpya ni miongoni mwa sera zao

Kauli hiyo ya jukwaa la katiba imekuja huku kukiwa na sintofaamu kuhusu kupatikana ama kutokupatikana kwa katiba mpya mchakato ambao ulisimama na kupisha uchaguzi mkuu mwaka 2015 na kuacha katika hatua ya Katiba Pendekezwa.
 
 
 
 
Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam Mratibu wa jukwaa la katiba Tanzania Ndugu Hebron Mwakagenda alisema wameshtushwa na kauli ya serikali ya Tano kuwa mchakato wa Katiba mpya sio kipaumbele cha serikali ilihali katika Ilani ya chama cha mapinduzi ndio Ilikuwa moja ya ahadi zao za kuhakikisha kuwa katiba hiyo inapatikana.


Mratibu wa JUKATA Ndugu Hebroni Mwakagenda akizungumza na wanahabari leo.