Zinazobamba

DC HAPI AIBUA MADUDU KINONDONI,NI YALE YA TASAF ,AMTUMBUA KIGOGO,SOMA HAPO KUJUA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjiJXKQseykufIhT_7-h-I_we7xWEaDHKuA6ZXuoMdnJvBBi0TB7-hQkPOigyzK9VcLJmg-YdwSlQsTN-qaX3QL18WyUPdjRtcdVQEhPwWtpmJrZ_-axR4iP8ffWqXABHGY269D-meYD-E/s1600/kipi.jpg
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi amemuagiza Mkurugenzi wa manispaa hiyo,Aron Kagurumjuli kumvua nyazifa za uongoni mratibu wa Mfuko wa Kusaidia kaya masikini(TASAF) katika wilaya kinondoni Onesmo Oyango baada ya kubainika  kuwaingiza kwenye malipo watu 1,397  ambao hawana sifa ya kuwalipwa fedha za hizo ambao wameghalimu zaidi ya milioni 266.9.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo

Hata hivyo,Hapi amewaomba viongozi wa Mfuko huo, ngazi ya taifa kumchukulia hatua pia mlipaji mkuu wa Taifa kwa hatua yake ya kuhusika kuwalipa watu hao, huku akijua hawana sifa ya kulipwa stahiki hizo.

Pamoja na hayo,Hapi pia ameiagiza Taasisi ya kuzuia na kupamba na Rushwa (TAKUKURU)  katika wilaya yake kufanya uchunguzi wa kina kwa wanufaika wote na TASAF ili kujilizisha kama  wsanafuaika hao wanasifa za kupewa fedha hizo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam Hapi amesema baada ya  uchunguzi wa kina uliofanywa kwa wanufaika wote  wa fedha hizo ambao walitakiwa kunufaika ni watu masikini ambao hawana hata uwezo kuhudumia familia zao lakini wameshangazwa na hatua ya kulipwa watu wasiokuwa na sifa hizo
,
“Wamelipwa watu wenye uwezo sio  masikini au kaya masikini ambazo zilitakiwa kusaidiwa na mfuko huu “amesema Hapi.
Ameeleza kuwa mbali na watu hao wasikuwa na sifa pia wamebaini hata watu walionufaika na fedha hizo hawajulikana hata makazi wanapoishi jambo analodai limetia shaka ata fedha hizo, uwenda zilikuwa zinakwenda kwa wajanja wachache.
 “Lazima tumsadia Rais Joh Magufuli kupambana watu wote wanaofanya ufisadi kwa watendaji ,kwahiyo hapa naitaka (TAKUKURU) kufanya uchunguzi wa kina ,pamoja na taasisi za kinidhamu kwa wafanyakazi kwa watendaji hawa ili hatua zichukuliwe kwa wate waliohusika na kadhia hii”ameongeza Hapi