SAKATA LA ESCROW SASA LAWA PASUA KICHWA,TANESCO YAENDELEA KUNG'ANG'ANIWA,SOMA HAPO KUJUA
Benki ya Standard Chartered Limited ya Hong Kong
(SCB-HK) imefungua maombi Mahakama Kuu ikitaka, pamoja na mambo mengine,
Shirika la Umeme (Tanesco) lizuiwe kuilipa kampuni ya uzalishaji nishati
hiyo ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL).
Badala yake, SCB-HK inaomba malipo hayo yahifadhiwe
mahakamani hapo hadi Tanesco itakapolipa dola 148 milioni za Kimarekani (sawa
na zaidi ya Sh320 bilioni) kwa benki hiyo kama Mahakama ya Kimataifa ya Utatuzi
wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID) ilivyoagiza mwezi Septemba, tofauti na
ilivyokuwa wakati wa mgogoro wa Tanesco na IPTL wakati fedha zilipowekwa Benki
Kuu ya Tanzania (BoT).
Uamuzi wa ICISD ulikuja takriban miaka mitatu baada
ya Serikali kuidhinisha malipo ya takriban Sh306 bilioni kutoka akaunti ya escrow
iliyofunguliwa na Tanesco kwa kushirikiana na IPTL kusubiria uamuzi wa Mahakama
Kuu kuhusu mgogoro wa malipo ya tozo ya uwekezaji.
Mwaka 2005 SCB-HK, ilinunua deni ambalo benki ya
Danaharta ya Malaysia ilikuwa ikiidai IPTL baada ya kampuni hiyo kukopa dola
101.7 milioni za Kimarekani ili kununua mtambo wa ufuaji umeme wa Tegeta wenye
uwezo wa kuzalisha megawati 100. Lakini wakati fedha hizo zilipotolewa,
ililipwa kampuni ya Pan African Power Solutions (PAP), jambo lililofanya SCB-HK
kufungua kesi hiyo ICSID ikidai ndiyo iliyostahili malipo hayo, kesi ambayo
benki hiyo ilishinda.
Umuzi huo wa ICSID umeshakubaliwa na kusajiliwa na
Mahakama Kuu Tanzania kupitia maombi namba 687, ya mwaka 2016, yaliyofunguliwa
na SCB-HK, na hivyo unatambulika kama uamuzi wa mahakama hiyo.
IPTL inafua umeme ambao unauzwa kwa Tanesco.
Lakini SCB-HK imewasilisha maombi kwa hati ya
dharura ikiomba mahakama iizue Tenesco kuendelea kuilipa PAP, ambayo inamiliki
IPTL na badala yake pesa hizo ziwe zinahifadhiwa mahakamani hapo hadi deni hilo
litakapolipwa lote