Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imesema haitomfumbia
macho mtu, kampuni, wazabuni na makandarasi watakaolitia hasara jiji hilo
hususani kampuni zilizopewa tenda za ukusanyaji mapato.
Pia imesema haitatoa tenda za zabuni kwa kampuni zisizokuwa
na vigezo.
Hayo yamesemwa leo na Naibu Meya wa Jiji hilo, Mussa Kafana
wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utendaji kazi wa kampuni tatu
zilizoshinda zabuni za ukusanyaji kodi za maegesho katika halmashauri za
manispaa zilizomo katika jiji hilo.
Amezitaja kampuni zilizoshinda zabuni hizo kuwa ni, Kenya
Airport Parking Services katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala, Manispaa ya
Kinondoni ilishinda Ubapa, wakati Temeke ikishinda kampuni ya Upauka.
“Tumechaguliwa na wananchi ili kuwaletea maendeleo ambayo
yanatokana na mapato yanayokusanywa, hatotafumbia macho mtu yeyote
atakayesababisha hasara au kuruhusu mianya ya upotevu wa mapato,” amesema.
Aidha, Kafana amefafanua utendaji kazi wa kampuni hizo
baada ya kuwepo kwa malalamiko kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala haina
mzabuni wa kukusanya mapato ya maegesho kutokana kwamba aliyeshinda tenda hiyo
ambayo ni Kenya Airport Parking Services haijaanza kazi rasmi ya ukusanyaji
kodi na kwamba huenda manispaa hiyo ikapoteza mapato.
“Kampuni hizi tatu zilikidhi vigezo, ambapo ya Kenya
iliahidi kukuanya Bilioni 54 kwa mwaka na kwamba inatakiwa kukusanya milioni 20
kwa siku, ilitakiwa baada ya siku 28 ilete dhamana ya kazi ya asilimia 10 ya
fedha ilizoahidi kutoa kwa mwaka ambayo sawa na bilioni 5.4, lakini hadi sasa
haijatekeleza hilo na ndiyo sababu ya kutoanza kufanya kazi hadi sasa,”
amesema.
Kafana amewatoa hofu wananchi juu ya hilo kwa kusema kuwa
kampuni iliyomaliza muda wake imeombwa kuendelea kukusanya kodi za maegesho
hadi pale halmashauri itakapotafuta mzabuni mwingine.
Kuhusu utendaji kazi wa kampuni nyingine zilizoshinda
zabuni hiyo Temeke na Kinondoni, amesema zimeshaanza kufanya kazi.
HALMASHAURI YA JIJI YA DAR YAWA MBOGO KWA KAMPUNIZI ZA KITAPELI,NAIBU MEYA WA UKAWA ASEMA HAYA SOMA HAPO KUJUA
Reviewed by Unknown
on
19:15:00
Rating: 5