Zinazobamba

WAISLAM NCHINI WAHASWA KUPINGA UKANDAMIZAJI,SHEIKH ABDI ATOA NASAHA NZITO,SOMA HAPO KUJUA


Pichani ni
Naibu kiongozi mkuu wa waislam Shia Ithnasharia Tanzania Sheikh Muhammad Abdi akizngumza na wanahabari Leo Jijini Dar es salaam


 NA KAROLI VINSENT
WAISLAM nchini wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kupinga vitendo vyote vya dhuruma na ukandamizaji wanavyofanyiwa  raia, ili kujiwekea mazingira mazuri ya baadae.

Hata hivyo,Waislam pia wametakiwa kufanya mambo ya kumpendeza Mungu katika jamii inayowazunguka ili kuhakikisha wanawasaidi watu wasiojiweza.

Wito huo umetolewa leo Jijini Dar es salaam na Naibu kiongozi mkuu wa waislam Shia Ithnasharia Tanzania Sheikh Muhammad Abdi alipokuwa anazungumza na wanahabari kuhusu kuukaribisha mwaka mpya wa kiislam mwaka ambao ni wa 1438H katika kalenda ya kiislam pamoja na kumbukumbu ya Imam Hussein mkutano ambao umefanyika katika msikiti wao uliopo Kigogo Post Jijini Dar es salaam.

Amesema Waislam wanatakiwa kuongana na kupinga vitendo vya ukandamizaji na dhuruma vinavyotokea kwa jamii kama alivyofanya Imman Hussein ambaye alijitolea maisha yake kupinga vitendo vya ukandamizaji waliofanyiwa wananchi wa afrika ya kati.

“Tunapaswa kumkumbuka  Imman Hussein kwa miongoni mwa waislam waliokuwa mstari wa mbele kupinga dhuruma,kwani yeye hakupigania ubinadamu wa eneo ,linalomzunguka bali alihakikisha anapigania ubinadamu wa Dunia nzima,jambo hili linatakiwa kuigwa na waislam wote”amesema Sheikh Abdi.
Sheik Abdi ameongeza kuzungumza kwa uchungu,amesema Imam Hussein ambaye wanamkumbuka leo ni moja kati ya viongozi wa dini ambao aliwafunza watu namna ya kupinga ukandamizaji,dhuluma katika jamii pamoja na kutetea haki za wanyonge hivyo ni wakati wa wananchi wa Tanzania kuanza kufwata maneno yake na kuhakikisha kuwa wanaenzi yale mema aliyoyaacha katika jamii.
Kiongozi huyo wa kiroho amesema  kuwa leo hii dunia inalazimika kuitika wito wa Imam Hussein ili kuinusuru dunia iliyotapakaa damu kila kona,ambapo akitolea mfano wa mashariki ya kati ambapo imekuwa ikishughudiwa watoto wanavyochinjwa na maelfu kukimbia makazi yao kwa sababu ya uharibifu,
Huku pia katika bara la Africa ikishughudiwa makundi ya kiigaidi yakiibuka katika nchi nyingi ambapo yamekuwa yakileta madhara makubwa kwa wananchi wasio na hatia huku  akisema kuwa mambo haya ni mambo ambayo yalikuwa yanamkera sana Imam Hussein na kama angekuwepo angejitokeza kupambana nayo