Zinazobamba

BALAA LILOMKUTA FREEMAN MBOWE,SASA KUMKUTA SUMAYE,SERIKALI YAJIPANGA KUMCHUKULIA MALI ZAKE,SOMA HAPO KUJUA



http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2697148/medRes/708602/-/juwewbz/-/suma_frederick.jpg
NA KAROLI VINSENT
WAKATI ikiwa imepita mwezi mmoja baada ya serikali kupitia shirika la Nyumba la Taifa(NHC) kuiondosha kwenye jengo la shirika hilo, kampuni ya Freemedia ambayo inamilikiwa na mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Freeman Mbowe kwa  madai ya kudaiwa Bilioni 1.6 ambapo mali zake zikiwa zinatakiwa kuuzwa kwa mnada
 kufidia deni hilo.

 Sasa “Songombingo” kama hilo linaanza kumyemelea  Waziri mkuu mstaafu wa awamu ya tatu,Fredrick Sumaye,ambapo sasa serikali kupitia kwa afisa Ardhi wa manispaa ya Kinondoni kumwandia hati ya barua ya siku 90 ya kumtaka ajieleze kwanini ameshindwa kuliendeleza Shamba lake lilioko Bunju ndani ya manispaa hiyo kabla hajanyang’anywa eneo hilo na serikali.

Waziri wa Nyumba na Maendeleo na Makazi,William Lukuvi amewasibitishia waaandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuwa teyari Manispaa ya Kinondoni imeshamwandikia hati ya barua ya siku 90 ya kujieleza kwa Sumaye ambaye pia ni mwanachama wa Chama cha Chadema.

“Ninachowaambia katika suala la Ardhi hatuangalii kama wewe ni mkubwa au mdogo,kama umeshindwa kuliendeleza eneo tunakunyang’anya,kuhusu huyu Sumaye tumemwandikia hati ya barua ya siku 90 na kumtaka ajieleze kwanini ameshindwa kuliendeleza kwa mda mrefu,na kama akishindwa kutoa maelezo ya kueleweka basi tutamnyang’anya kwa kumfutia hati ya kumiliki shamba hilo”amesema Lukuvi.

Kauli hiyo ya Lukuvi inakuja ikiwa ni teyari Sumaye ambaye ni Waziri mkuu peke aliyedumu katika kipindi cha miaka 10 madarakani kuriko mawaziri wakuu wote kuwai tokea nchini,ambapo inaeleza Sumaye aliwai kulalamika  kupitia vyombo vya habari kuwa serikali inataka kumpora ardhi yake kwa kile alichokiita kisa “yeye yupo vyama vya Upinzani”

Maamuzi hayo ya Lukuvi yanakuja  sambamba ikiwa ndani ya   shamba hilo la Sumaye  kuibuka mgogoro mkubwa kati yake na wananchi waliovamia shamba lake kwa kile wananchi hao  wanachokisema “shamba hilo halijendelezwa “ ndio maana wamelivamia.

Akizungumzia hali hiyo, Kigogo mmoja aliyokoa ndani ya serikali ya Magufuli ambaye aliomba jina lake lisijitajwe mtandaoni ,amesema hatua  hiyo ya serikali ipo kisiasa tu.

“Tatizo hii nchi inakuwa masikini kutokana na  siasa tu ndugu ,hivi ni watu wangapi wapo ndani ya CCM wanamiliki mashamba makubwa tena hawajaendeleza hawanyang’anywi,leo ndio wanamuona sumaye tu,hapa wanataka kumkomoa tu”

“Kwanza Sumaye anavielezo tosha kuwa pale anataka kujenga Chuo kikuu na amechelewesha kwa sababu ya kuweka mipango kamili,lakini siasa za majitaka za Taifa hili wanakata kumkomoa tu,hapo Sumaye akapambane nao mahakamani tu haki yake ataipata tu”amesema Mtoa taarifa huyo.