Zinazobamba

MAUZO KATIKA SOKO LA HISA YASHUKA KWA ASILIMIA 81,MARRY KINABO ASEMA CHANZO,SOMA HAPO KUJUA




Idadi ya mauzo ya Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE) imeshuka kwa asilimia 81 kutoka bilioni 9 na kufikia 1.7 bilioni katika kipindi cha wiki iliyopita.

Hayo yamesemwa leo na Afisa Masoko Mwandamizi wa DSE Marry Kinabo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.
 
“Idadi ya mauzo imeshuka kwa asilimia 81 kutoka bilioni 9 na kufikia 1.7 bilioni, pia idadi ya zilizouzwa na kununuliwa zimeshuka kwa asilimia 68 kutoka milioni 1 hadi 340,000,” amesema.
Amesema pia ukubwa wa mtaji wa soko umeshuka kwa asilimia 2.79 kutoka trilioni 21 na kufikia 20.7 trilioni. Ukubwa wa mtaji wa makampuni ya ndani umebaki kwenye kiwango kilekile cha Panda 8.2 trilioni.
Aidha, Kinabo ametaja kampuni tatu zilizoongoza kwa idadi ya zilizouzwa na kununuliwa katika kipindi cha wiki iliyopita kuwa ni CRDB kwa asilimia 53, TBL asilimia 35, na Swissport kwa asilimia 3.
“sekta ya viwanda wiki ilkyoisha imeshuka kwa alama 36.6 baada ya bei za hisa za TBL kushuka kwa asilimia 1.08. Sekta ya huduma za kibenki na kifedha imepanda kwa pointi 3.64 baada ya bei kpanda kwenye kaunta za DSE kwa asilimia 11.57,” amesema.
Pia amesema sekta ya huduma za kibiashara kwa wiki iliyopita imeshuka kwa pointi 4.19 baada ya bei kupanda kwenye kaunta za Swissport.