Zinazobamba

KAMPUNI YA KUJENGA BARABARA YA DEL-MONTE YAENDELEA KUKATALIWA JIJINI DAR,NAIBU MEYA WA ILALA AUNGANA NA RC MAKONDA,SOMA HAPO KUJUA



Pichani ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala,Omary Ngumilamoto akifafanua jambo na waandishi wa habari(Picha na Maktaba)


NAIBU meya wa Manispaa ya Ilala,Omary Ngumilamoto amesema wataiondoa kwenye tenda Kampuni ya  ujenzi wa Barabara Del-Monte  katika manispaa hiyo baada ya kujiridhisha kampuni hiyo inafanya kazi chini ya kiwango ikiwemo kuchelewesha kumaliza kazi kwa wakati.Anaandika KAROLI VINSENT  endelea nayo,

Kauli ya Ngumilamoto inakuja ikiwa ni tayari mkuu wa mkoa wa Dare s Salaam,Paul Makonda  ambaye naye aliiagiza viongozi wote wa manispaa ya mkoa huo kutoipa  tenda kampuni ya Del-Monte kutokana na kujenga barabara nyingi chini ya kiwango.

Ngumilamoto ambaye ni Diwani wa Kata ya Vingunguti kupitia chama cha Wananchi (CUF) ameyasema hayo leo wakati alipokuwa anafanya ziara na Kamati ya fedha ya Manispaa hiyo kwenye miradi mbali mbali iliyoanza kutekelezwa ili kujilidhisha juu ya ufanisi wake. 

Amesema Kampuni hiyo ilipewa tenda ya kujenga barabara kutoka Mombasa hadi Mosha Baa kwa kiwango cha Lami ambayo inaurefu wa kilomotea 1.65 ambayo itagarimu Bilioni Sh 2.4  ambapo kwa sasa kampuni hiyo imepewa milioni 301,

“Hii Kampuni ya Del-monte tulishakamtaa kutokana na miradi mingi tunayompa kushindwa kumaliza miradi kwa wakati  licha ya kupewa fedha lakini bado anatusumbua”amesema Ngumilamoto,
Ngumilamoto amesema Halmashauri hiyo ilishaingia Mkataba na kampuni hiyo hivyo hawezi kumkatisha mkataba wake,ila amedai kuwa Mkataba wake ukishamalizika  hawataendelea nayo kampuni hiyo  ikiwemo kuipa  tenda tena katika Halmashauri hiyo.

Sanjari na hayo,pia Ngumilamoto amemtaka Kaimu Mhandisi wa Manispaa hiyo,Nyamagulula Masatu kuhakikisha anasimamia miradi huo uwe unakamilika kwa wakati na kuisimamia ipasavyo kutokana na kuwepo kwa miradi mingi ya Barabara kuharibika hata mwaka mmoja haujamilizika.

Kwa Upande wake Mhandisi Masatu alimuhakikishia Ngumilamoto kuwa ataisimamia  mradi huo na kuhakikisha itaisha kwa wakati.