MREMA AJIFICHA KWENYE KIVULI CHA LOWASSA,SOMA HAPO KUJUA
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema akiwa anatafakari bungeni |
HATUA ya Augustino Mrema, Mwenyekiti wa Chama cha
TLP kutajwa kama wakala wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ndani ya upinzani,
inamkera, anaandika Regina Mkonde.
Mrema ambaye hivi karibuni Rais
John Magufuli ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Parole amesema, yeye si CCM B na
kwamba, ikiwa hivyo basi Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea urais kupitia Chama
cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mwaka jana, anapaswa kuitwa CCM
B.
“Kama
ni hivyo, basi na Lowassa ni CCM B, si alihama mwaka jana,” amesema Mrema leo
kwenye mkutano wake na madereva wa bodaboda katika Wilaya ya Kinondoni, Dar es
Salaam.
Lowassa
alihamia Chadema mwaka 2015 baada ya kuonekana kile kilichoitwa mizengwe ndani
ya CCM hasa baada ya jina lake kuondolewa kabla ya kupigiwa kura ya uteuzi wa
mgombea ngazi ya urais katika kukiwakilisha chama hichi kwenye Uchaguzi Mkuu wa
mwaka jana.
Mrema
amekuwa akipata wakati mgumu kujitetea pale anapohusishwa na harakati zake za
kisiasa kwamba, amekuwa akitumikia CCM zaidi ya upinzani.
“Hata
angekuja Lowassa, ningemuuliza mwaka ule nilipofukuzwa nilimwambia tuhamie
upinzani wote, akakataa hadi alipojitoa mwaka jana CCM,” amesema na kuongeza;
“Sumaye
(Frederick Sumaye, Waziri Mkuu Mstaafu) naye alikuwepo, nilimwambia njoo huku.
Waliposhindwa kuteuliwa kuwania urais waliondoka, halafu wanasema mimi ni CCM
B, wao nani.?”
Mrema
mesema, alilazimika kumpigia kampeni Rais Magufuli katika Uchaguzi kwa imani
kuwa, ndiye aliyemuona anafaa.
Katika
hatua nyingine, Mrema amempa siku saba Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam kumueleza sababu ya madereva wa bodaboda kufanya shughuli zao maeneo ya
mjini yaliyokatazwa.
“Natoa
siku saba, nataka kujua Makonda hao waliofanya shughuli hizi sehemu
zilizokatazwa, wanafanya hivyo kwa niaba ya nani?” amehoji Mrema na kuongeza;
“Makonda
nakwambia, kama unajifanya huna macho na huoni, huna masikio na husikii, mbona
ukiona majipu unakuwa mwepesi kuyatumbua, kwa nini jipu hili la pikipiki pale
mjini hulitumbui? Kwa sababu hali hii ikiendelea ni sawa na ubaguzi.”
Pamoja
na agizo hilo Mrema amesema “sina nia ya kumfitinisha Makonda bali inachotaka
kuona ni utendaji wa kazi unaozingatia haki kwa madereva hao.