TCRA YAVIPIGA PINI VITUO VYA EATV NA REDIO YA E.FM,NI MWENDELEZO WAKE SOMA HAPO KUJUA
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgg8k8Sp7euFzGvAztgsUsMGNKhv3uxfUN1D0tBnyc3kU6j71VwakCdNWMMpJBTpx3AqUTfJ4v2dKqxR-9XRPveNS8DE8f1YV1k0WvQ7wGcXWqwG3lnQ3bmIE6smYrGdKP8VXBZg9drRSg/s1600/TCRA+logo.png)
MAMLAKA Ya Mawasiliano nchini (TCRA) imevitoza faini
vituo viwili vya Utangazaji ambavyo ni Entertment Fm (E.FM) faini ya Milioni 4
pamoja na kituo cha Luninga cha East African Television (EATV) faini ya milioni 3 baada ya kukiuka kanuni za utangazaji.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo
Akisoma hukumu hiyo mda huu Makao Makuu ya (TCRA) yaliopo Jijini Dar es Salaam,Kaimu mwenyekiti
wa Kamati ya Maudhui ya Mamlaka hiyo,Joseph Mapumba amesema vituo hivyo
vimekiuka sheria ya utangazaji ya mwaka 2005 baada ya kufanya makosa ya
udhalilishaji kwa wanawake pamoja na
kuchochea imani za ushirikina.
Mapunda ametaja makosa ya vituo hivyo, amesema mnamo
tarehe 16/5/2016 kituo cha EATV katika kipindi cha muziki ambacho kilirusha
majira ya saa 9.30 usiku kipindi hicho kilicheza Wimbo wa panya ambao umeimbwa na msanii Blacketi ambaye
amemshirikisha Msanii Tecno.
Amesema Wimbo huo ulikuwa unamaudhui ya
kumdhalilisha mwanamke kutokana na video hiyo kumwonyesha mwanamke akiwa “uchi”
yaani hana nguo. Kwa kuvaa vazi la ufukweni huku akiwa hana nguo.
Amesema kituo hicho kilitenda kosa la kuonyesha
video hiyo mda ambao bado watoto wapo macho jambo analosema linakwenda na kinyume na sheria ya utangazaji
ya mwaka 2005 inayotaka vipindi vya aina hiyo kuwekea mda maalum yaani wa
usiku.
Amesema mara baada ya Kamati hiyo kubaini makosa
hayo waliwasiliana na uongozi wa EATV ambapo mkurugenzi wake,Regilna Mengi alitoa utetezi wake kwa kusema video hiyo
ilikuwa haina makosa kwani vazi ambalo mamlaka hiyo wanalosema lilikuwa ni
kumfedhesha mwanamke ni vazi ambalo linavaliwa ufukweni huku akisemwa hapa
nchini hakuna sheria inatoa mwongozo wa vazi gani livaliwa kwenye ufukwe.
Amesema mara baada ya kusikiliza utetezi ndipo
kamati imeamua kituo hicho kupewa onyo kali kutokana na kukiuka kanuniza za
utangaji ya mwaka 2005 pamoja na kuambiwa walipa faini ya milioni 3.
KOSA LA
REDIO YA E.FM.
Mapunda pia ametaja makosa yaliyofanya na E.FM
redio,ambapo redio hiyo ilikiuka sheria hizo katika kipindi cha Ubaoni
kinachorushwa kwaanzia saa 10 jioni hadi saa 1.00 ,ambapo amesema kipindi hicho
cha tarehe 13/4/2016 ,mtangazaji wa kipindi hicho, alifanya mahojiano na binti
ambaye alijitamburusha kuwa amefanya mauaji kwa kutumia imani za kishirikina.
Mapunda amesema binti huyo alisema amefanya
ushirikina kwa kumuua mototo wa bosi wake huku akidai kuwa amesaidiwa na bibi
yake.
Amesema kipindi hicho iimekiuka sheria ya utangazaji
kwa hatua yake anayodai inachochea watu kujiingiza kwenye imani za kishirikina.
Amesema mara baada ya kubaini kosa hilo,Kamati yake
iliwasiliana na wamiliki wa Redio hiyo ambayo katika utetezi wake uliwasilishwa
na Mhariri mkuu wa E.FM,Scholastika Mazula ambaye alisema katika kipindi hicho hakulioni kosa
bali kipindi hicho kilikuwa na lengo ya kueleza ubaya wa imani za
kishirikna kwa jamii.
Mapunda amesema mara baada ya Kamtai hiyo kusikiliza
utetezi huo,ndio wakabaini kituo hicho kilikiuka sheria ya utangazaji ya mwaka
2005 inayokataza kurusha vipindi vitakavyohalibu umoja na mshikamo wa taifa.
Amesema Kamati hiyo imetoa hukumu ya kupiga faini ya
Milioni 4 pamoja na kuipa onyo kali ambapo endapo kituo hicho kikikaidi basi
hawatasita kuichukulia hatua kali.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni