Zinazobamba

PROFESA LIPUMBA AUMBUKA RASMI,RAIS MAGUFULI AMWACHA "SOLEMBA",SOMA HAPO KUJUA



John Magufuli, Rais wa Tanzania


NA KAROLI VINSENT
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF)Profesa Ibrahimu Lipumba ni kama ndoto yake imefutika ya kuwa mshauri wa uchumi wa Utawala wa Rais John Magufuli baada ya Rais huyo kumteua  Profesa Longinus Rutasitara kuwa mshauri wa Rais masuala ya uchumi.

Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa  ya Ikulu kwa Vyombo vya habari inasema Profesa Rurasitara ameteuliwa kushika nafasi hiyo,ambaye kabla ya kuteuliwa nafasi hiyo alikuwa mhadhili wa kitivo cha uchumi kutoka Chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
Kuteliwa kwa msomi huyo wa uchumi,kunazidi mwacha “solemba”Profesa Lipumba ambaye alijiaminisha mara baada ya kujiuzulu nafasi ya uenyekiti mwaka jana wakati wa kipindi cha Kampeni kwa kile alichokiita ni kutoridhika kwa ujio wa Lowassa kugombania Urais kupitia vyama vinavyounda UKAWA.

Profesa Lipumba ambaye mara kuikacha nafasi hiyo ilisemekana kuwa sababu ya kuachia nafasi hiyo ilitokana na kuhadiwa nafasi ya ushauri wa uchumi kwa serikali ya aliyekuwa mgombea wa Urais wa Chama cha Mapinduzi CCM ambaye sasa ni Rais, ili kuudhofisha upinzani.
Akizungumza kwa kujiamini Kigogo Mwandamizi kutoka chama cha CUF ambaye alikataa jina lake kutajwa kwenye mtandao huu alisema kutoteuliwa kwa Lipumba kwenye nafasi hiyo itakuwa ni fundisho kwa wanasiasa mandumilakuili.
“Ninachokwambia huyo bwana (Lipumba) alichofanyiwa itakuwa itakuwa fundisho kwa wanharakati wengene waoaaacha kutetea mabadiliko kisa kuahidiwa vitu hewa,nazani amejifunza acha yamkute”amesema kigogo huyo.
Mbali na Mshauri huyo wa Uchumi,pia Rais Magufuli amemteau Naibu Mwanasheria mkuu wa Serikali  Gerson Mdemu kushika nafasi hiyo ambayo hapo awali ilishikwa na Apson Tulia ambaye sasa ni Naibu spika wa Bunge l;a Jamhuri wa Muungano wa Tanzania