Zinazobamba

SHEIKH JALALA AWATAKA WAISLAMU KUWEKEZA KATIKA TAFITI

Kiongozi Mkuu wa Chuo cha Kiislam (Hawzat) Imam Swadiq (a.s) Sheikh Hemed Jalala akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa kujisomea na kufanya tafiti kwa Masheikh mbalimbali waliohudhuria hafla ya Kuzindua maktaba ya Maarifa  hivi karibuni huko Kariakoo   
Sehemu ya Waislamu waliohudhulia uzinduzi wa Maktaba mpya kabisa Jijini Daresalaam Wakimsikiliza Sheikh Jalala akifafanua kuhusu umuhimu wa kusoma na kufanya Tafiti.
Hapa Sheikh Jalala akizindua maktaba hiyo mpya. Maktaba hiyo inatarajiwa kuwahudumia Watanzania wote wenye malengo ya kujifunza zaidi elimu ya dini.
Kiongozi Mkuu wa Chuo cha Kiislam (Hawzat) Imam Swadiq (a.s) Sheikh Hemed Jalala ameitaka jamii ya Kiislamu kuwekeza katika tafiti kwani kufanya hivyo kutasaidia kufahamu mambo mengi katika ulimwengu wa sasa.

Akizungumza katika uzinduzi wa maktaba  ya Maarifa Jijini Daresalaam, Sheikh Jalala amesema njia pekee ya kuifahamu jamii na kuweza kufikisha ujumbe wa Mungu kwao ni kufanya Tafiti.
Sheikh Jalala amesema ni wakati sasa Masheikh na wanazuoni kuona umuhimu wa kuwekeza katika Elimu hususani sekta ya Tafiti ili kuweza kwenda sambamba na karne ya sasa.

Akizungumzia umuhimu wa kufanya Tafiti, Sheikh amesema Toka enzi hizo suala la Tafiti lilikuwa linafanywa na Waislamu lakini miaka ya hivi karibuni dhima hiyo imekuwa kama imepokwa kwani suala la tafiti limekuwa likifanywa Zaidi na Wazungu.

Akizungumzia umuhimu wa Masheikh wa hapa nchini kufanya Tafiti, Sheikh Jalala amesema kuna umuhimu mkubwa kwa Masheikh wetu kujikita katika kufanya Tafiti kwani kutasaidia kutambua changamoto zinazoikabili jamii.

Amesema Masheikh wakifanya Tafiti na kuja na maandiko mbalimbali kama vile Vitabu na Makala katika magazeti mbalimbali itasaidia kuleta athari katika jamii na hivyo kusaidia kuisukuma dini ya Uislamu mbele.

 “Niwaombe Masheikh wenzangu na vijana kujituma na kusoma kwa bidii ili kuisaidia jamii yetu, lazima tujenge utamaduni wa kufanya tafiti ili ziweze kuwasaidia huko mbele ya safari” Alisema 

Aidha katika hatua nyingine, Wafuasi wa Shia Ithnasheriya Tanzania wametumia nafasi ya ufunguzi wa Makataba hiyo mpya kusheherekea siku ya kuzaliwa kwa Imam Mah’d (a.t.f.s) ambaye ni Kiongozi wa 12 baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w) anayetarajiwa kurudi tena duniani hapo baadae na kuleta Amani na Maelewano kwa watu.

Sheikh Jalala amesema Waislam wote Duniani wanaamini ya kwamba Dunia hawezi Kumalizika mpaka aje mtu, mtu huyo atakapo kuja atawaokoa wanadamu, kwenye matatizo na dunia ataibadilisha kuwa kisiwa cha amani, Maelewano, Mshikamano na kuhakikisha dhuma na Ufisadi unasambaratika duniani.

“Shaabn 15 siku kama ya leo (Jana) mwaka 255 Hijiria alizaliwa Imamu wa 12 wa watu wa nyumba ya Mtume (saw). Jina lake kamili ni Muhamad, lakini majina yake mengine ni Mahdi, Sahib uz Zaman. Al-Hujjah, baba yake alikuwa Imamu wa 11 Imam Hassan al-Askari (as) na Mama yake alikuwa Nargis Khatoon” hivyo Leo tunasheherekea hilo.
 Suala la Itikadi ya Imam mahd limekuwa likizua utata mkubwa sana baina ya Madhehebu ya waislamu duniani”                         

Hakuna maoni