Zinazobamba

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA ALIPULIWA,CHAMA CHA ADC CHAMJIA JUU,SOMA HAPO KUJUA


Pichani ni
Naibu katibu mkuu wa chama cha ALLIANCE FOR DEMOCRATIC CHANGE ADC Ndugu DOYO HASSAN DOYO akionyesha baadhi ya nyaraka mbalimbali ambazo zinaonyesha jinsi msajili wa Vyama vya siasa alivyokiuka katiba ya chama hicho katika maelekezo yake ya kutaka mwenyekiti wa chama hicho arejeshwe madarakani baada ya kutimuliwa na Bodi ya wadhamini ya chama hicho


CHAMA cha Alliance for Democratic Chance (ADC) kimemtaka msajili wa Vyama vya siasa nchini,Jaji Francis Mtungi kuacha kupandikiza migogoro ndani ya chama hicho.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
 
Hatua ya Chama cha ADC kufikia hatua hiyo imetokana na Ofisi ya Msajili  kuendelea kuutambua uongozi wa aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Said Miraaj Abdulla,ambapo uongozi huo uliosimamishwa na chama hicho kutokana na kile kinachodaiwa kuwa amekiuka kanuni za chama.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam,Naibu Katibu mkuu wa ADC Bara ,Doyo Hassani Doyo  amesema chama hicho tarehe 27/4/2016 kilipokea barua kutoka kwa msajili wa vyama vya siasa inayo utambua uongozi uliosimamishwa.

Amesema baada ya chama hicho kupokea barua hiyo walibaini barua hiyo imekuwa na upungufu mkubwa na kuishusha hadhi ofisi ya msajili.
Wanahabari wakiwa kazini


“Barua hiyo ya msajili haikuzingatia matakwa ya katiba yetu ya ADC,zaidi  ya kubabea ushabiki wa msajili na ishara ya wazi na kutaka kuendeleza mgogoro  ambao teyari tulishaupatia ufumbuzi,lakini msajili hana hoja zenye msingi  tena  inaonekana anamaslahi na uongozi anautetea”amesema Doyo.

Doyo amedai kuwa chama chake kimchukulia hatua Bwana Said Miraaj Abdulla,ni kutokana na kukiuka kanuni za chama kwa kitendo chake cha kuongea na waandishi wa habari na kuongea mambo yanahusu chama hicho bila ya kupata idhini ya chama hicho kama katiba inavyoelekeza.

Hata Hivyo, chama cha ADC kimemtaka Msajili wa vyama vya siasa aache kubeba uongozi wanaodai kuwa sio wa kihalali  kwa ni umesimamishwa kwa mujibu wa chama hicho kifungu  kidogo (1) h cha Katiba  ya chama hicho.

“Katiba inasema  endapo kwa sababu ya yoyote  ile chama kitakosa uongozi halali wa kikatiba au kitakuwa na mgogoro wa uongozi  na  kukifanya kukosa uhalali  wa kufanya shughuli zake,bodi ya wadhamini wa chama kwa mujibu wa kifungo hichi itakuwa na mamlaka ya kamili ya kusimamia shughuli za uendeshaji hadi hapo chama kitakapopata uongozi halali”amesema Doyo.

Katika hatua nyengine chama hicho kimemtaka Rais John Magufuli kuzingatia sheria ya nchi katika kubadilisha matumizi wa fedha kama alivyofanya pale alipofuta sherehe za uhuru pamoja na muungano kwa kuidhinisha pesa zile kwenda kwenye matumizi mengine.

Hakuna maoni