Zinazobamba

MIRAJI AMLIPUA HAMADI RASHIDI...AMTAKA ATOKE HADHARANI




Hatimaye Mwenyekiti wa Chama Cha Alliance for democratic Change(ADC)Saidi Miraaji,amemtaka Hamad Rashid aache tabia ya kutumia vibaraka kuleta migogoro ndani ya chama badala yake atoke hadharani wapambane kwa hoja.
Akizungumza na Waandishi wa habari, Miraaji amesema sababu ya mgogoro wa chama ni Hamadi Rashidi,amekuwa akifanya uvurugaji wa katiba na kanuni ya chama kwa kutumia vibaraka wake
 “Nataka nimwambie Hamadi Rashidi atoke hadharani apambane na mimi, kuendelea kuwa nyuma ya pazia huku akifadhili vikao ambavyo vinalenga kunivua uenyekiti havitaweza kushinda kwa sababu chama kinaongozwa kwa misingi ya katiba na Kananu”
Amesema hata ukiangalia rekodi za Hamadi Rashid amekuwa ni mtu wa kufukuzwa kwa kila chama anachoingia na hiyo inadhihirisha jinsi ambavyo alivyokuwa mvurugaji wa mambo.
Akizungumzia kuhusu sakata la yeye kutimuliwa amesema yeye hana hana nia ya kung’ang’ania uongozi lakini anachofanya ni kutaka kuonyesha umma kuwa kinachofanyika katika Chama cha ADC si haki
Amesema kwa hali ilivyo hata waende wapi hawataweza kushinda na kwamba atapambana kuona haki zake zinapatikana, kwani anaamini kinachofanywa na viongozi waliopo ni kinyume cha katiba ya chama


                                                                                                
Nafahamu HAMAD RASHID anatamani leo kesho akamate nafasi ya uenyekiti katika chama cha ADC lakini kwa jinsi anavyokwenda anajiharibia, naona mwisho nwa mwanasiasa huyu unakaribia”Alisema Miraji.
Amesema kuwa tangu kumalizika kwa uchaguzi wa awali visiwani Zanzibar HAMAD RASHID ambaye alikuwa mgombea wa chama hicho Visiwani Zanzibar amekuwa akitoa matamko yanayokihusu chama bila kuwashirikisha viongozi halali wa chama hicho likiwemo tamko la kukubali kushiriki katika uchaguzi wa marudio wa Zanzibar tamko ambalo amesema halikuwa na Baraka za chama hicho.

MIRAAJ amewaeleza wanahabari kuwa yeye kama mwenyekiti wa chama alimpokea  HAMAD RASHID kama mwanachama wa kawaida na baadae kukubali awe mlezi wa chama hicho kutokana na ukongwe wake katika siasa za Tanzania lakini hawakumpa kazi ya usemaji wa chama kwani kwa mujibu wa katiba ya chama hicho msemaji pekee wa chama hicho ni mwenyekiti.

Aidha Ameeleza kuwa kazi pekee ya mlezi wa chama ni kuwashauri viongozi wakuu wa chama na sio kutoa maamuzi ya chama kama aliyoyafanya ya kukubali kurejea uchaguzi wa Zanzibar bila ridhaa ya mwenyekiti na vyombo husika vya chama,huku akimtaka aache kuivuruga katiba ya chama hicho.

Amesema kuwa kwa mujibu wa katiba ya chama hicho baraza la wadhamini la chama halina nguvu yoyote kisheria ya kumuondoa mwenyekiti madarakani kamali livyofanya hivyo yeye ataendelea kuwa mwenyekiti wa chama hicho hadi pale ambapo itaamuliwana na sheria kuwa hafai kuwa mwenyekiti huku akisema anajipanga kwenda kwa msajili wa vyama vya siasa hapo kesho kumweleza masikitiko yake ya kuzuiwa na watu ambao amewaita wahuni ndani ya chama kurejea katika ofisi zake kama kawaida.

Hapo jana Naibu katibu mkuu wa chama hicho DOYO HASSAN DOYO aliwaeleza wanahabari kuwa mwenyekiti huyo haruhusiwi kufika katika eneo lolote la ofisi za chama hadi apate mwaliko maalum wa chama hicho tamko ambalo mwenyekiti huyo SAID MIRAAJ amelikanusha na kusema kuwa limeandikwa kihuni na wahuni wanaotaka kukivuruga chama na yeye hayupo tayari kuwavumilia.

Ameongeza kuwa tamko la chama hicho kwa wanahabari la jana halina uhalali kwa kuwa limeandikwa kihuni bila saini ya mwandikaji,bila jina la mwandikaji hivyo hakuna tamko la chama linalotoka hivyo.
Mgogoro ndani ya chama hicho uliibuka mara tu baada ya kumalizika kwa uchaguzi wa kwanza wa Zanzibar ambapo swala la uchaguzi wa marudio liliwagawa viongozi hao huku ikionekana wazi kuwa mwenyekiti huyo hakuwa tayari chama cha ADC kushiriki katika uchaguzi huo huku mgombea HAMAD RASHID ambaye ameonekana kuwa na nguvu ndani ya chama hicho kushiriki katika uchaguzi huo uliopelekea chama cha mapinduzi kuibuka na ushindi mnono.

Hakuna maoni