MAUZO KATIKA SOKO LA HISA YAPUNGUA,MUSUSA ATAJA CHANZO CHAKE,SOMA HAPO KUJUA
Pichani ni Meneja Mauzo na
Biashara wa (DSE) |
MAUZO
katika Soko la Hisa Mkoani Dar es Salaam, (DSE) yameshuka kwa asilimia 59
kutoka sh.bilioni 6.84 kwa wiki iliyopita hadi kufikia shilingi Bilion 2.8 kwa
wiki hii.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo,
Hata
hivyo, Idadi ya hiyo ya hisa zilizouzwa na kununuliwa zimeshuka kwa
asilimia 26 kutoka milioni 3.8 hadi kufikia Milioni 2.8.
Patrick Mususa ambaye ni Meneja Mauzo na
Biashara wa (DSE) Amewaambia waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam,kuwa kiwango hicho cha mauzo
kimeshuka katika soko hilo kumechangiwa
na kupungua ukubwa wa Sekta ya huduma za kibeki na kifedha kwa pointi 7.87.
Mususa pia amezitaja kampuni zilizoongoza kwa mauzo katika soko hilo ni pamoja na Benki ya CRDB kwa Asilimia 92.40, ikifwatiwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kwa asilimia 4.16 na Benki ya maendeleoya wakulima (MBP) kwa asilimia 1.61.
Mususa
amesema ukubwa wa mtaji wa Soko umebaki kwenye kiwango kile kile cha Trilioni
22 ambapo wa mtaji wa makampuni ya ndani umeongezeka kwa asilimia 1 hadi kutoka
Trilioni 8.4 hadi kufikia Trilioni 8.4.
Aidha Mususa amebainisha kuwa Viashiria katika Sekta ya viwanda vimeongezeka kwa pointi 36.26 baada ya bei za hisa za TOL na TBL kupanda kwa asilimia 3.75 na 1.14 ambapo sekta ya huduma za kibiashara zimebaki kwenye kiwango kile kile cha sh. 3,697.92.
Sanjari na hayo,pia Mususa amesema jumla ya wanafunzi Vyuo Vikuu waliojiunga katika shindano la (Scholar Investment Challenge 2016) linalo endeshwa na taasisi hiyo wamefikia 3,160 kutoka katika vyuo mbalimbali nchini.
Mususa amefafanuwa
Hakuna maoni
Chapisha Maoni