IDADI YA MAUZO KATIKA SOKO LA HISA YAONGEZEKA,MUSUSA ATAJA CHANZO,SOMA KUJUA
Pichani ni Meneja Mauzo na Biashara wa (DSE),Patrick Mususa akizungumza na Waandishi wa habari(Hawapo pichani)kuhusu hali ya mauzo katika soko hilo |
NA KAROLI VINSENT
MAUZO ya Soko la Hisa Mkoani Dar es Salaam (DSE) kwa
wiki hii yameongezeka kwa asilimia 76 kutoka sh.bilion 2.8 kwa wiki iliyopita
hadi kufikia sh. bilioni 4.9 kwa hiki hii,
Huku pia Idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa kwa
wiki hii zimeshuka kwa asilimia 20,Milioni 2.2 kutoka Milioni 2.8.
Akizungumza Dar es Salaam leo Meneja mauzo na Biashara wa (DSE), Patrick Mususa amesema kuongezeka kwa mauzo katika soko hilo kumechangiwa na idadi kubwa ya wafanya biashara kujitokeza kununua hisa hizo
Hata hivyo,Mususa ameyataja makampuni yaliyoongoza katika wiki ni pamoja na Benki NMB kwa asilimia 47.85, CRDB asilimia 38.34 na kampuni ya Swissport asilimia 10.00.
Mususa pia ametaja ukubwa wa mtaji wa soko umeongezeka asilimia 0.5 kutoka Trilioni 22.0 hadi Trilioni 22.1 ambapo ukubwa mtaji wa makampuni ya ndani umepungua kwa asilimia 0.1 kutoka Trilioni 8.5 hadi kufikia Trilioni 8.4
Aidha Mususa amesema Sekta ya viwanda (IA) imepungua kwa pointi 2.72 ambapo huduma za kibenki na kifedha
(BI) zimeshuka kwa pointi 10.36 baada ya bei kushuka kwenye kaunta za CRDB kwa asilimia 1.33 wakati huduma za kibiashara (CS) nazo zimeshuka kwa pointi 16.75 baada ya bei kushuka kwenye kaunta ya SWISSPORT 0.59.
Akizungumza Dar es Salaam leo Meneja mauzo na Biashara wa (DSE), Patrick Mususa amesema kuongezeka kwa mauzo katika soko hilo kumechangiwa na idadi kubwa ya wafanya biashara kujitokeza kununua hisa hizo
Hata hivyo,Mususa ameyataja makampuni yaliyoongoza katika wiki ni pamoja na Benki NMB kwa asilimia 47.85, CRDB asilimia 38.34 na kampuni ya Swissport asilimia 10.00.
Mususa pia ametaja ukubwa wa mtaji wa soko umeongezeka asilimia 0.5 kutoka Trilioni 22.0 hadi Trilioni 22.1 ambapo ukubwa mtaji wa makampuni ya ndani umepungua kwa asilimia 0.1 kutoka Trilioni 8.5 hadi kufikia Trilioni 8.4
Aidha Mususa amesema Sekta ya viwanda (IA) imepungua kwa pointi 2.72 ambapo huduma za kibenki na kifedha
(BI) zimeshuka kwa pointi 10.36 baada ya bei kushuka kwenye kaunta za CRDB kwa asilimia 1.33 wakati huduma za kibiashara (CS) nazo zimeshuka kwa pointi 16.75 baada ya bei kushuka kwenye kaunta ya SWISSPORT 0.59.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni