BREAKING NEWS,MEYA WA UKAWA KINONDONI ATUMBUA VIGOGO,WAKUTWA NA UFISADI WA KUTISHA,SOMA HAPO KUJUA
Meya wa Ukawa Manispaa ya Kinondoni,Bonifacce Jacob |
BARAZA la Madiwani wa Manispaa ya Kinondoni wameridhia
hatua ya kumsimasha kazi Mwanasheria
mkuu wa Manispaa hiyo Burton Mahenge pamoja na Mthamini wa Manispaa hiyo Eihard
Chidaga kutokana kuingia mikataba ya utata
ambayo imetia hasara Halmashauri hiyo bilioni zaidi ya Bilioni 7.Anaandika
KAROLI VINSENT endelea nayo
Akitangaza uamuzi huo mda huu Jijini Dar es Salaam mbele ya wanahabari,Meya
wa Manispaa ya Kinondoni,Boniface Jacob amesema uamuzi huo wa kuwasimamisha
watendaji hao umetokana na kikao cha
madiwani kilichokaa jana, kimebaini Ubadhilifu kwenye mikataba iliyoingiwa na
watendaji hao na kuisabisha Halmashauri hiyo kupata hasara.
Jaccob ametaja makosa hayo yaliyogundulika ni mradi
wa uwekezaji wa Oysterbay Villa ulioko jijini hapa ambao mradi huo umeikosesha
halmashauri hiyo milioni 900 kwa mwaka lakini kutokana na mgogoro uliopo
umeikosesha manispaa hiyo shilling
bilioni 4.5 kwa miaka mitano tangu mradi huo kuanza.
Amefafanua kuwa mradi huo ulikamilika tangu 2011
katika viwanja vyote viwili Na.277na 322 ambapo uwekezaji wake katika kiwanja
277 una nyumba Na 322 Nyumba 68 lakini amedai kuwa mwekazaji huo wa nyumba
hizo hajazilipia kodi.
Sanjari na hiyo,pia Jaccob ambaye ni Diwani wa
Ubungo ametaja kosa jingine lilofanywa na Viongozi hao kuwa ni mogogoro wa
upangaji wa nyumba za Magomeni Kata umetokana na Mwansheria huyo kuingia Mkataba
na wapangaji waliokuwepo katika eneo hilo ambapo mkataba huo unata kulipwa fedha ya milioni
1.080000 kwa mwaka wapangaji hao licha ya kuhama
katika eneo hilo.
“Yaani huyo Mwanasheria ameingia mkataba Bogus
treaty (mikataba ya kijinga) ambao kwa mwaka tunawalipa wapangaji hawa milioni moja kwa mwaka wakati
wameshahama katika eneo hili,kwahiyo kwa
uzembe wa mkataba huo sasa hivi manispaa tunadaiwa zaidi ya bilioni 3 kwa mwaka”amesema Jaccob,
Hata hivyo,Jaccob amesema baada ya Halmashauri hiyo kugoma kuwalipa fedha hizo,wapangaji hao wamekwenda kufungua Kesi Mahakamani na kutolewa hati ya Kukamatwa Mkurugenzi wa Manispaa hiyo Aron Kagurumjuu,
Ameleza kuwa licha ya Hati hiyo kutolewa lakini Mwanasheria huyo alishindwa kumtaharifu Mkurugenzi wake wakati alikuwepo mahakamani jambo analosema linazidi ibua utata.
MKATABA WA
COCO BEACH.
Jaccob amesema Mahenge pia anahusika katika sakata
la mkataba tata wa Coco beach kutoka na kitendo chake cha kuzembea mpaka serikali
ikashindwa kesi mahakamani kwa hatua yake ya kutofika mahakamani wakati wa kesi hiyo ikisomwa, jambo analodai lilichangia mahakama kuipa ushindi kampuni Q-Consult limited ambayo
ni ya Mwenyekiti wa Klabu ya mpira ya Yanga,Yusufu Manji kuendelea na uwekezaj.
Licha kushindwa huko mahakamani pia Mahenge
amepuuzia agizo la Rais John Magufuli lilotaka kesi hiyo ikatiwe rufaa lakini
Mahenge tangu 2015 hukumu hiyo ilipotolewa hajakata rufaa mapaka sasa jambo
linalotia mashaka uwenda naye anamslai ya Kampuni hiyo.
MRADI WA
UJENZI WA MADUKA YA MAKUMBUSHO (EASTERN CAPITAL LTD)
Jaccob amedai
kuwa madiwani hao wamebaini utata kwenye kituo hicho cha mabasi kilichopo
makumbusho baada ya kugundulika halmashauri inapata mapato madogo ya milioni 4 kwa
mwezi tofauti na mapato ya milioni 40 kwa mwezi kwenye kituo cha awali
cha Mwenge.
Amefafanu kuwa mkataba huo wa makumbusho Halmashauri inapata asilimia 15 huku Mbia
anapata asilimia 85 ya mkataba huo jambo linalolikosesha fedha Halmashauri na kupelekea kuibua utata ya sababu ya kuhama kituo cha Mwenge chenye mapato makubwa.
Amedai kuwa katika eneo hilo pia kuna jengo la gorofa huku jengo hilo limeongezwa gorofa mbili
ambazo amedai kuwa halmashauri hizo haipati fedha huku ujenzi wake ukiwa
tofauti na mkataba unavyotaka kwani ulitaka kuwa na gorofa moja.
Jaccob ametaja
miradi mengine ya kiufisadi waliofanya watendaji hao ni Ujenzi wa Nyumba za
Makazi Hill ostarbei ambao amedai kuwa
tangu mkataba huo usainiwa 2009 ,huku mkataba huo ukibadilisha matumizi ya
awali ya mkataba huo bila halmashauri kutalifiwa taarifa za ubadilishaji huo.
Nyingine ni ujenzi za Nyumba za Makazi kwanja Na.314
toure drive ambapo mkataba huo
unatekelezwa na ubia na kamapuni ya lake Oil limited na mradio huo unaonekana kuingiwa mwaka 2019
ambao mda haujafika,
Licha kudanganya mwaka pia mkataba huo unaoenkana
umefanyiwa marekebisho bila kufuta idhini ya halmashauri na kuishabisha mradi
kuchelewa kuanza na kupelekea kuiskosesha mapato serikal.
Vilevile,Jacob amesema baada ya kuwasimaisha watendaji hao,hautua inayofuata ni kuwachunguza na kuwapeleka mahakamani,huku akizitaka makampuni ya uwakili yalipo kwenye wilaya hiyo kujitokeza wakati viongozi hao watakapowapeleka mahakani ili watoe msaada wa kisheria.
A
Licha ya Kampuni hizo,pia Jacoob ameitaka Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kushirikana nao katika kuchunguza mikataba yote ambayo imeingiwa na watendaji hao kwani inaviashiria vya ufisadi.
Vilevile,Jacob amesema baada ya kuwasimaisha watendaji hao,hautua inayofuata ni kuwachunguza na kuwapeleka mahakamani,huku akizitaka makampuni ya uwakili yalipo kwenye wilaya hiyo kujitokeza wakati viongozi hao watakapowapeleka mahakani ili watoe msaada wa kisheria.
A
Licha ya Kampuni hizo,pia Jacoob ameitaka Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) kushirikana nao katika kuchunguza mikataba yote ambayo imeingiwa na watendaji hao kwani inaviashiria vya ufisadi.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni