Zinazobamba

MAZAZI YA IMAM ALI KUNA SOMO LA KUJIFUNZA-SHEKHE JALALA



Imeelezwa kuwa ikiwa ni kipindi cha takribani karne 14 zimepita toka kutokea kifo cha mwanafunzi wa Mtume Muhammad (Rehma na Amani ziwe Juu yake), Waislamu na wasio Waislamu wametakiwa kuusoma utawala wa Imam Ali kwani katika utawala huo kuna mambo mengi ya kujifunza yatakayosaidia kuwatendea haki wananchi tunaowaoongoza.
Akizungumza na FULLHABARI BLOG  katika kumbukizi ya Mazazi ya Imam Ali ofisini kwake, kiongozi mkuu wa Chuo cha Kiislamu (Hawza) Immam Swadiq Sheikh Hemed Jalala, alisema kuna somo kubwa la kujifunza katika utawala Imam Ali.
Shekhe Jalala alitaja baadhi ya mambo muhimu ambayo unaweza kuyapata katika utawala wake ni jinsi ambayo alikuwa akiongoza umma wa watu huku akimtanguliza Mungu.
Alisema Utawala wa Imam Ali ulitawaliwa na hofu ya Mungu jambo ambalo lilisaidia kupunguza vitendo vya ufisadi, vitendo vya kuminya haki za binadamu na watu wengi kuwa na moyo wa kuwajibika.
Alisema Enzi zake, viongozi walikuwa na hofu ya Mungu, kila mtu alikuwa anafanya kazi kwa moyo wake bila kubagua rangi jinsia na dini husika.

“Niwape kisa kimoja, Enzi zake Imam Ali wakati akiwa anatembea tembea akiwa barabarani akamuona mzee akiwa anaombaomba akauliza vipi huyu; Wasaidi wake wakamwambia yule ni yahudi akasema wakati akiwa na nguvu zake hamkuyaona hayo sasa, naagiza kuanzia leo mtu huyu awe analipwa mshahara na serikali”
Kisa hicho kinaonyesha ni jinsi gani asivyokuwa mbaguzi, na kwamba watawala wanapaswa kutokuwa wabaguzi kama alivyo Imam Ali.
Aufananisha Utawala wa Magufuli na Imam Ali
Katika hatua Nyingine, Sheikh Jalala ambaye pia ni Kiongozi mkuu wa Waislamu dhehebu la shia Ithnasheria amesema kama linakuja suala la kufafanisha uongozi basi kwa mbali utawala wa Magufuli unaonekana kufuata nyayo zake.
Sheikh Hemed Jalala amesema hatua zinazochukuliwa na Rais Magufuli zinafanana kwa mbali na Imam Ali ambaye mara nyingi alikuwa anachukizwa na watu kutowajibika katika majukumu yao.
Ukimuangalia Rais Magufuli amekuwa akitumia muda mwingi kuhakikisha serikali yake inakuwa na watu wachapa kazi, waliokuwa tayari kuwatumikia watu badala ya matumbo yao.

 “Ndugu zangu nataka nitumie fursa hii kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Rais John Magufuli, bila shaka kwa kasi anayoenda nayo taifa litapiga hatua kubwa na kufanya wananchi wa hali ya chini kunufaika na rasilimali zilizopo”
Alisema Ukimsoma Imam Ali (Mwanafunzi wa Mtume Muhammadi Rehma na Amani ziwe juu yake) utagundua kuwa katika utawala wake hakupenda wananchi wa hali ya chini kunyanyasika, na pia alitilia mkazo wa watu wake kutafuta elimu popote pale.
Amesema jambo hilo pia limeonyesha kwa vitendo na Rais wa awamu ya Tano Rais John Joseph Pombe Magufuli hususani pale alipotangaza kuwa Elimu bure hadi kidato cha nne.


Hakuna maoni