KUMEKUCHA HALMASHAURI YA KINONDONI,UKAWA WAANZA KULETA NEEMA,MEYA WAKE AZIDI BUNI MIKAKATI,SOMA KUJUA
Meya wa Halmashauri Manispaa ya Kinondoni,
Boniface Jacob wa (kushoto) akimkabidhi mkataba Meneja wa Tawi la Gauff
Consultants, Thorsten Seitz.
|
MANISPAA ya Kinondoni na Kampuni GAFF ya nchini
Ujerumani wameingia mkataba wa kushauri na kubuni ujenzi wa miundombinu na
miradi ya maendeleo (DMDP) kwenye manispaa hiyo,
Akizungumza na waandishi wa
habari leo kabla ya kusaini mkataba huo Boniface Jacob, Mstahiki Meya wa
Manispaa hiyo amesema kuwa, mshauri huyo mwelekezi wa mradi huo utakaoghalimu
Sh. 50 bilioni, atafanya utafiti wa jinsi ya kujenga miundomibinu ya barabara
kwenye manspaa hiyo. Mtandao wa FULLHABARI.BLOGS umeshuhudia uingiaji mkataba
huo.
Jacob
ambaye ni Diwani wa Kata ya Ubungo (Chadema) amesema kuwa, fedha zimetolewa na
Benki ya Dunia ili kudhamini miradi hiyo na kwamba, miongoni mwa miradi hiyo ni
ujenzi wa barabara 13 ambazo zitadumu kwa zaidi ya miaka 20.
Akitaja
baadhi ya barabara amesema ni Barabara ya Maji ya Chumvi hadi Korogwe,
Mburahati hadi NIT, Manzese Darajani hadi Urafiki.
Jacob
amesema kuwa, kwa mara ya kwanza manispaa hiyo itaujengea Mto wa Ng’ombe na Mto
Msimbazi kwa teknolojia ya kisisasa ili kuzuia maafa.
“Mradi
huo utahusisha ujenzi wa Mto Msimbazi kuanzia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam hadi
Hananasifu ambapo manispaa itawalipa fidia wakazi walio karibu na mto huo ndani
ya mita 30,”amesema Jacob.
Thorste
Sertz, Maneja wa Kampuni GAFF Tawi la Tanzania amesema kuwa, atahakikisha
anabuni miradi itakayoifanya kinondoni kuwa na miundombinu mizuri.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni