Zinazobamba

HATIMAYE USAFIRI WA TRENI KUTOKA DAR HADI MWANZA NA KIGOMA WAREJEA,TRL YASEMA HALI IPO SAFI,SOMA HAPO KUJUA



Pichani ni Afisa Habari wa TRL,Midraji mahezi akizungumza na waandishi wa habari leo,Jijini Dar es SalaaM


KAMPUNI ya Reli nchini (TRL) imerejesha katika hali yake usafiri wa Treni  ya Deluxe kutoka Bara hadi Kigoma pamoja na maeneo mengine ya nchi.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.

Kurejea usafiri huo kutokana  na kutengemaa kwa eneo korofi baina ya stesheni za Kilosa mkoani Mgorogoro na Gulwe Mkoani Dodoma ambapo maeneo hayo yalikuwa korofi kutokana na  mvua zinazonyesha maeneo hayo na kupelekea kuharibika  miundombinu ya reli.

Akizungumza na Waandishi wa Habari kwaniaba ya Kaimu mkurugenzi  Mtendaji wa TRL Masanja Kadogosa,Afisa Habari wa TRL Midladjy Maez amesema kwa mujibu wa Taarifa kutoka kwa wakuu idara za uendeshaji wa Kampuni hiyo  iliyotolewa Aprili 26 mwaka huu  baada ya kufanya ukaguzi wa kina katika  eneo  la Gulwe wamejiridhisha kuwa hali imetengemaa.

“Wachunguzi wetu wamesema eneo la Gulwe kwa sasa linapitika kutokana na kuimalika kwa tuta na kuwezesha treni zote za abiria na mizigo kupita kwa usalama kabisa”amesema Maez.

Maez ametoa mchanganuo wa  safari za Treni pamoja mda wake ambapo Safari za kawaida kutoka Dar es Salaam kuelekea Mwanza na Kigoma itaanza siku ya  Jumanne Mei 3,2016,huku Treni ya Dulexe itaondoka Dar es Salaam kila siku ya Jumapili saa 2.00 usiku.

Hata Hivyo,Maez ameleza kuwa Treni ya kutoka Mwanza na Kigoma kuja Dar es Salaam itatoka huko kila siku ya Alhamisi na Jumapili kwaanzia mda wa 11.00 jioni na saa 12 jioni kwa Mwanza,huku Treni ya Dulexe nayo itatoka Kigoma au Mwanza kila siku ya Jumanne saa 2.oo usiku.

Pamoja na hayo,Maez aliwataka wasafiri wote kufanya utatibu wa Safari mapema (booking) katika stesheni za TRL na sio mahara pengine.

Hakuna maoni