Zinazobamba

WAISLAM WAITOLEA LAWAMA SERIKALI YA SAUDI ARABIA,NI BAADA YA VIFO VYA MAHUJAJI,SOMA HAPO KUJUA

Pichani ni Mwalimu na msomi wa katika theologia ya Uislam wa umoja wa Mahujaji Shehe Abdulmalik Swaleh ambaye –
        naye alikuwa miongoni mwa mahujaji wa kitanzania waliokwenda kuhiji akizungumza na waandishi wa habari.

NA KAROLI VINSENT
 HUKU kikiwa bado haijafamahika idadi harisi ya Mahujaji wa kitanzania walifariki nchini Saudi Arabia,nao viongozi wa dini wa dhehebu la shia  nchini wameibuka na kuilahumu serikali ya nchini Saudi Arabia kwa kupelea vifo hivyo.
    Akizungumza na waandishi wa habari mda huu Jijini Dar es Salaam,Mwalimu na msomi wa katika theologia ya Uislam wa umoja wa Mahujaji Shehe Abdulmalik Swaleh ambaye –
        naye alikuwa miongoni mwa mahujaji wa kitanzania waliokwenda kuhiji,ambapo amesema vifo hivyo vya kusikitisha vya watu wanaofikia elfu nne zimesababishwa na serikali ya Saudi Arabia kutoweka mazingira mazuri kwa mahujaji hao.
         Amesema hata miundombinu ya barabara katika nchi hiyo zilikuwa ndogo sana ukizingatia na idadi kubwa ya watu waliokwenda kuhiji,
 “Serikali ya Saudi Arabia inapaswa kupewa lawama,mahujaji tulikuwa wengi sana kuriko hata miundomini ya barabara iliyokuwepo,watu tulikuwa tunakanyagana harafu hali ya joto ndio maana hata vifo hivyo”
Viongozi wa Dhehebu ya Shia wakitoa malalamiko kwa serikaliya Saudi Arabia

          Aidha, Shekh Swalehe ameitupia pia lawama tena serikali ya nchi hiyo,kwa kubadirisha mfumo mzima uliozoeleka wa kwenda kuhiji,

“Hata mfumo wa kuhiji umebadirika sana,kwani wakati tunakwenda  kutupia jiwe shetani tulikuwa tunatupa jiwe harafu tunaondokea kwa njia hiyo hiyo,ila sahivi tunashangaa sana tunakwenda baada ya kutupa jiwe tunarudi njia hiyo hiyo kwahiyo unakuta watu walikuwa nyuma yetu tunagongana na kuanza kukanyaganya”amesema




Hakuna maoni