Zinazobamba

SERIKALI YACHARUKIA PICHA HIZI.NI ZILE ZA TWIGA KUSAFIRISHWA,YAIBUKA NA KUSEMA HAYA,SOMA HAPO KUJUA


WIZARA ya Maliasili na Utalii imesema hakuna Twiga yeyote  aliyetoroshwa toka kwenye mbuga za wananyama na kupelekwa nje ya nchi katika kipindi hiki.Anaadika KAROLI VINSENT endelea nayo.
     Kauli hiyo ya wizara inakuja kukiwa na picha mbali mbali zikiwa zimeenezwa kwenye mitandao ya kijamii zikionyesha uwepo wa Ndege kubwa ndani ya mbuga za wanyama huku picha hizo zikionyesha watu watano wakiwa wanampakiza Twiga kwenye Ndege kama ambavyo unaziona hapo.
      Akitoa ufafanuzi wa picha hizo,Katibu mkuu wa Wizaya ya Maliasili na Utalii Dk Adelhelm Meru  leo Jijini Dar Es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari ambapo amesema picha hizo ni za kutengeneza kwani hakuna mnyama yeyote aliyesafirishwa kwenda nje.
“Watu wamekuwa wanatumia suala hili kisiasa kwa kupakua picha za internet kutoka nchi zingine wanazitengeneza na kusema za hapa nchini”amesema Meru
           Amesema kuwa “Twiga ni nembo muhimu kwa Taifa letu,hairusiwi kuwindwa na kusafirishwa mnyama huyo”
Aidha Dk Meru amekiri kuwepo na wageni kutoka nchi za nje,wanaokuja kuwinda katika mbugu zetu jambo analodai limekuwa likiliingiza Taifa mapato makubwa.
Amefafanua kuwa katika kipindi hiki mfalme mmoja kutoka nchi za kiarabu alikuja kufanya uwindaji kwa mda wa siku nne yaani toka Semptemba 24 hadi 29.
       



Amesema Mfalme huyo alikuwa na watu wengine 137 ambao walikuja na Ndege tatu ambazo zilishuka katika uwanja wa Kilimanjaro (KIA) ambapo pia hapo waliacha ndege mbili moja waliongozana nao hadi kwenye mbugani.



Hakuna maoni