Zinazobamba

TAFITI :ZOEZI LA KUANDIKISHA WAPIGA KURA KWA MFUMO WA BVR HALIJAFANIKIWA TANZANIA


Mwenyekiti wa mtandao wa Asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini TACCEO Bi MARTINA KABISAMA akifafanua jambo kwa wanahabari mapema leo

Makamu mwenyekiti wa TACCEO Bwana ISRAEL ILUNDE akifafanua mambo kadhaa ambayo mtandao huo uliyashughudia wakati wa zoezi la uandikishwaji
 
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC Bi HELLEN KIJO BISIMBA akifafanua jambo mbele ya wanahabari baada ya kuwasilishwa kwa report nzima ya TACCEO juu ya mchakato wa uandikishwaji wa wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa BVR

  Imeelezwa kuwa zoezi la uandikishwajiwa wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa kielekronic BVR limekuwa si la mafanikio kutokana na kasoro nyingi kulikumba zoezi kwa ujumla

Hayo yameibuliwa na Mtandao wa asasi za kiraia wa kuangalia chaguzi nchini Tanzania TACCEO mapema hii leo wakati wakitoa report yao ya kitafiti kuhusu zoezi la uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mfumo mpya wa kielectronic BVR lilivyoendeshwa
 
Akizungumza na wadau mbalimbali pamoja na wanahabari Jijini Dar es salaam Mkurugenzi mtendaji wa Kituo cha sheria na haki za Binadamu Dk Hellen Kijo Bisimba  amekili kuwa tafiti za TACCEO zimeonyesha kutofanikiwa kwa zoezi la uandikishwaji licha ya tume ya taifa ya uchaguzi kusisitiza kuwa zoezi hilo lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa
 
Akizitaja kasoro moja wapo iliyokuwa kikwazo kikubwa katika mchakato wa uandikiswaji ni kukosekana kwa elimu mahususi ya mpiga kura juu ya zoezi la auandikishwaji na umuhimu wa zoezi lenyewe jambo ambalo amesema kuwa limekuwa ni kikwazo kikubwa kwani wananchi wengi walikuwa hawaelewi nini maana ya mchakato huo huku wengine wakiwa hawataki hata kujiandikisha kwa kuhofia kuwa kuna mbinu mbalimbali zinatumika ili kupata taarifa zao.


Amesema kuwa maeneo mengi kulikuwa na usumbufu mkubwa wa wananchi kaumini kwa mashine zile zilikuwa na madhara kwa afya zao,wengine wakiamini kuwa wanapimwa virusi vya ukumwi bila kujijua huku wengine wakiamini kuwa zoezi lile ni maswala ya kishirikina yakihusishwa pia na imani za kishetani za Fremason huku wengine wakiamini kuwa wakiwa na vitambulisho vile vya awali haikuwa na haja ya kujiandikisha upya, jambo ambalo amesema kuwa yote hayo ni kutokana na kukosekana kwa elimu ya mpiga kure kipindi cha zoezi la uandikishwaji.

Chanagamaoto nyingine ambayo TACCEO wamekiri kukutana nayo wakati wa zoezi hilo ni waandikishaji wa zoezi hilo ikiwa  na maana ya mawakala waliopewa kazi ya kuandikisha kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya matumizi ya mfumo huo pamoja na mashine husika jambo ambalo wamesema kuwa lilikuwa ni changamoto kubwa kwa wafanyakazi hao na kusababisha zoezi hilo kwenda kwa kusua sua hali ambayo wamedai ilijitokeza katika kila eneo nchini Tanzania.

Dk Hellen Kijo Bisimba amesema kuwa changamoto nyingine ambazo zilikuwa zikiukumba mchakato huo ni pamoja na ubovu wa mashine ambao ulisababisha zoezi kuahirishwa mara kwa mara,wanafunzi kukosa haki yao ya kujiandikisha,pamoja na matatizo ya kiuhakiki ambapo watu waliokuwa hawapati nafasi ya kuhakiki taarifa zao kabla ya kupewa kitambulisho jambo ambalo limesababisha watu wengi kupewa vitambulisho ambavyo vina taarifa ambazo sio za kweli.
Wadau
Akizungumza na wanahabari mwenyekiti wa TACCEO Bi MARTINA KABISAMA amesema kuwa ni lazima tume ihakikishe kuwa inarekebisha kasoro zilizojitokeza katika mchakato wa uandikishwaji wa BVR ili usijirudie tena wakati wa uchaguzi jambo ambalo litasaidia uchaguzi kuwa wa huru na haki kwa watanzania wote


Hakuna maoni