Zinazobamba

TAASISI YA CARE$ HELP YAJA NA HICHI KWA VIJANA ,SOMA HAPO KUJUA



TAASISI ya Care & Help kwa kushirikiana na Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) na Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya Tanzania, imewataka Watanzania kuongeza nguvu ya ziada katika kusimamia maisha ya vijana wa kike na kuboresha maisha yao.        
Hayo yamesemwa leo katika mjadala wa kongamano la kujadili changamoto zinazowakabili wanawake lililofanyika chini ya taasisi isiyo ya kiserikali ya Care and Help inayolenga kumkomboa msichana katika majanga hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Uradibishi katika TACAIDS, Jacob Kayombo amesema matatizo mengi ya wasichana yanatokana na mfumo wa utamaduni usiompa haki ambazo hupelekea vishawishi.
         Kayombo amesema miongoni mwa utamaduni mbovu uliojengeka ni mwanamke kushiriki shughuli zinazoingiza kipato kidogo na kupigwa na hata kusababisha ulemavu.
    Amesema kuwa wanawake wakipewa elimu ya haki na usawa itabadilisha maisha yao hivyo kuwa katika nafasi nzuri na kuepuka vishawishi malimbali.
      Pichani ni Ofisa Elimu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za kulevya,Moza Makumbuli akizungumza kwenye Seminia hiyo


Ofisa Elimu wa Tume ya Kuratibu Udhibiti wa Dawa za Kulevya, Moza Makumbuli amesema matumizi ya Dawa za Kulevya yanaathari kubwa hasa kwa upende wa wanawake ikiwa ni pamoja na kujiuza.
Makumbuli amesema kuwa licha ya uwezekano mkubwa wa wanawake kuathirika lakini kwa sasa tiba yao inapatikana katika hospitali za mikoa.


Hakuna maoni