NEC YAMTULIZA JOHN MNYIKA,NI KUHUSU DAFTARI LA KUPIGA KURA SOMA HAPO KUJUA
TUME ya Taifa
ya Uchaguzi nchini NEC imesema majina ya wapiga kura yaliyopo kwenye Daftari la
kupiga kura yatabandikwa kwenye vituo vya kupiga kura siku nane kabla ya siku
ya kupiga kura ya octoba 25 mwaka huu.Anaandika KAROLI VINSENT endelea nayo.
Kuibuka
huku kwa NEC kunakuja siku moja kupita baada ya Naibu Katibu mkuu bara kupitia
Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, John Mnyika kuitaka tume hiyo
kupeleka Daftari hilo kwa wananchi mara moja,lasivyo wangeandamana hadi ofisi
za NEC.
Akizungumza
na waandishi wa Habari leo Jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Uchaguzi kutoka
ndani ya NEC,Profesa Chaliga amesema Tume yake imesikitika juu ya tuhuma
anazotoa Mnyika kuhusu Daftari hilo huku akisema kanuni za uchaguzi,
Ni kwamba
majina ya wapiga kura yanabandikwa kwenye vituo vya kupiga kura siku nane kabla
ya siku ya uchaguzi.
Amesema
nia ya kubandika majina hayo siku nane kabla ni kuweka usalama ili
yasibanduliwe.
“Jamani
anavyosema tunabandike leo kwenye vituo ni makosa kwani tukiyandaika leo mpaka
siku yenyewe ya kupiga kura si yatakuwa
yamebanduka,ndio maana tunaweka siku nane kabla,kwahiyo wanasiasa wasipotoshe
hili”
Profesa
Chaliga amesema kwa sasa hatua zinazoendelea ni tume hiyo kupeleka daftari hilo
kwenye mikoa tofauti nchini.
Naye
Mwenyekiti wa NEC Jaji mstaafu Damian Lubuva amewataka watanzania ,kujitokeza
siku ya kupiga kura na kuwachagua
viongozi wanaowataka baada ya hapo wanatakiwa kurudi nyumbani na kuacha kukaa
kwenye vituo vya uchaguzi kwa madai ya
kulinda kura,amedai katika uchaguzi
huu hakuna kura yeyote itakayoibiwa.
Hakuna maoni
Chapisha Maoni